• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

ZIARA YA WAHESHIMIWA MADIWANI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MVOMERO WILAYANI KYELA YALETA NEEMA KWA WAKULIMA WA KAKAO

Posted on: January 2nd, 2025

Waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero wamefanya ziara ya kimkakati katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya kwa lengo la kujifunza mbinu bora za kilimo cha kakao na kuongeza tija kwa wakulima wa zao hilo katika wilaya yao. Ziara hiyo imekuwa na manufaa makubwa kwa wakulima wa kakao wa Mvomero, kwani imefungua fursa mpya za kuboresha uzalishaji na kuongeza kipato cha wakulima.

Ziara hiyo iliyoanza Januari 2, 2025 imehusisha kikao cha mafunzo na maonyesho ya teknolojia mpya za kilimo cha kakao katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, ambayo inasifika kwa uzalishaji wa kiwango kikubwa na cha ubora wa kakao nchini. Madiwani hao walipata nafasi ya kujifunza kuhusu mbinu za kisasa za upandaji, usimamizi wa mashamba, uchakataji wa mazao, na mbinu za kufikia masoko ya kimataifa.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe. Jailos Msigwa kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, amesema kuwa wamejifunza mambo mengi ambayo yatahamasisha mabadiliko makubwa katika sekta ya kilimo cha kakao Mvomero. Ameongeza kuwa mikakati madhubuti itachukuliwa kuhakikisha wakulima wa kakao wanapatiwa mafunzo na vifaa bora vya kilimo.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela Mhe. Ambakisye Njelekela amewashukuru Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kwa kuichagua wilaya yao kama eneo la mafunzo na kubainisha kuwa ushirikiano kati ya wilaya hizo mbili utasaidia kukuza kilimo cha kakao kitaifa.

Naye Afisa Kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Bw. Mohammed Longoi amesema Halmashauri hiyo ina kitalu cha zao hilo la Kokoa ambapo msimu wa mwaka 2023/2024 ilizalisha miche 2700 ambayo iligawanywa kwa wakulima lakini mwitikio wake haukuwa mkubwa. Aidha, amebainisha kuwa kwa msimu wa mwaka 2024/2025 wakulima wameonesha kuwa na mwamko mkubwa. Sambamba na hilo amewapongeza Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri hiyo kwa kujitoa kujifunza kilimo cha zao hilo ili kuhakikisha kuwa maisha ya wakulima yanabadilika.

Akitoa taarifa ya hali ya uzalishaji wa zao la kokoa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, Afisa Kilimo wa Halmashauri  Mhandisi Arnold Ngaiza amesema kuwa Kilimo cha kokoa kimekuwa chanzo kikubwa kimojawapo cha kipato cha Halmashauri hiyo akitolea mfano msimu wa mwaka 2023/2024 Halmashauri imekusanya mapato kiasi cha shilingi Bilioni 2.1. Aidha, Mhandisi Arnold amesema Wilaya hiyo inazalisha mazao matatu ya kimkakati yakiwemo mazao ya Kakao, michikichi na mpunga.

Kwa ziara hii, Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero wameonesha dhamira ya dhati ya kuinua uchumi wa wakulima na kuboresha hali ya maisha kupitia kilimo cha kakao.


MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.