• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

Maendeleo ya Jamii

KAZI NA MAJUKUMU YA VITENGO

 UTANGULIZI 

Idara ya Maendeleo ya Jamii ni miongoni mwa Idara kati ya Idara zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero . Hii ni Idara mtambuka ambapo lengo lake kuu ni kuelimisha wananchi katika mambo mbalimbali ya kijamii, kiuchumi na kisiasa (kuratibu upatikanaji, usambazaji na utekelezaji wa Sera mbalimbali za Maendeleo). Kuhamasisha jamii kushiriki kwenye shughuli za maendeleo kwa lengo la kujiletea maendeleo yao wenyewe. Idara hii inaamini kwamba maendeleo ya mtu huletwa na mtu mwenyewe, ni imani yetu kwamba watu wanataka mabadiliko na wanaweza kubadilika, lakini hapa ifahamike kwamba mabadiliko yanayolengwa ni mabadiliko ya kimaendeleo na siyo vinginevyo.Idara ya maendeleo ya jamii ina vitengo 6 kama vilivyoainishwa hapa chini, kila kitengo na majukumu yake.

KITENGO CHA UTAFITI, TAKWIMU NA MIPANGO

Kukusanya takwimu mbalimbali za Halimashauri kwa matumizi ya idara

Kufanya uchambuzi wa takwimu

kutoa mafunzo ya uongozi na utawala kwa serikari ya vijiji na mitaa

Kufanya tafiti mbalimbali zenye kuiletea maendeleo jamii

Kuandaa maandiko ya mradi 

Uandaaji wa taarifa za robo mwaka na mwaka mzima za idara

Kusimamia kazi, shughuli na utendaji wa kazi wa Maafisa wa Maendeleo ya Jamii walioko kwemye kata

Kumshauri mkuu wa Idara mambo yahusuyo idara ya Maendeleo ya Jamii zikiwemo sera zote za idara na utekelezaji wake.

2. KITENGO CHA MAENDELEO YA WANAWAKE NA WATOTO.

Kusimamia mambo yote yahusuyo maendeleo ya wanawake na watoto katika Halmashauri,

kuratibu sherehe ya siku ya wanawake Duniani,

kuratibu sherehe ya siku ya mtoto wa Afrika,

Kuunda na kuhamasisha uanzishaji wa vikundi vya kiuchumi vya wanawake,

Kusimamia mfuko wa maendeleo ya wanawake kwa utoaji wa mikopo na marejesho yake,

Kutoa taarifa ya maendeleo ya mfuko wa wanawake,

Kusimamia sera za maendeleo ya wanawake na watoto,

Mshauri wa mkuu wa idara juu ya masuala yote yahusuyo maendeleo ya wanawake na watoto.

3. KITENGO CHA MAENDELEO NA JINSIA

Kuelimisha jamii dhana ya jinsia na kuratibu sherehe ya siku ya familia,

Kuelimisha jamii juu ya dhana potofu ya mila na desturi zinazoathiri jamii kimaendeleo,

Kutoa elimu/mafunzo na uhamasishaji wa dhana ya lishe kwa jamii kwaajili ya kuleta maendeleo katika jamii,

Mshauri wa mkuu wa idara juu ya sera na utekelezaji wake kwa masuala yote yahusuyo jinsia,

4. KITENGO CHA USTAWI WA JAMII

Kusimamia utambuzi wa watoto walioko katika mazingira hatarishi kwa kuwa na takwimu za mara ( yatima, watoto wa mtaani),

Kufanya utambuzi wa makundi maalumu kama wazee,wajane,wagane,wenye ulemavu

kuratibu sherehe ya siku ya wazee Duniani

Kutoa huduma (service delivery) kwa jamii/familia zenye migogoro ya ukosefu wa huduma za watoto

Kuielimisha jamii juu ya sheria ya mtoto, ajira za watoto

Kusimamia utaratibu wa PAROLI- wafungwa wanaostahili kuwa nje ya magereza kwa kufanya kazi za kiserikali wakiwa kifungoni

Kuwa na mipango endelevu ya kupunguza kasi ya ongezeko la watoto wa mitaani

Kusimamia shughuli za ustawi wa jamii kwa wananchi/jamii

Kumshauri mkuu wa idara masuala yote yahusuyo ustawi wa jamii

5. KITENGO CHA UJENZI VIJIJINI

Kufanya utambuzi wa mafundi vijijini kwa fani zao(uashi,ufundi seremala ) pamoja na viwanda vidogo vidogo

Kutoa mafunzo ya mafundi juu ya ujenzi wa nyumba bora zenye gharama nafuu

Kuelimisha serikali za vijiji juu ya ujenzi wa makazi bora ya nyumba bora vijijini

Kusimamia upatikanaji wa ramani na usambazaji wa ramani za nyumba bora vijijini kwa serikali za vijiji

Kuunda vikosi vya ujenzi kwenye kata (building brigades) ili wasimamie kazi za ujenzi wa majengo ya serikali

Usambazaji wa teknologia sahihi kwa wananchi vijijini(majiko bora na banifu, zana bora za kazi)

Kumshauri mkuu wa idara masuala yote yahusuyo ufundi na ujenzi vijiji

6. KITENGO CHA VIJANA

Kuhamasisha juu ya sera ya vijana

Kushirikiana na Afisa utamaduni juu ya masuala ya maedndeleo ya vijana

Kuhamasisha uundaji wa vikundi vya vijana

kusimamia utoaji mikopo kwa vijana na marejesho yake

Kufanya utambuzi wa vikundi vya vijana na shughuli zao za kiuchumi

Kutoa elimu/ mafunzo ya ujasriamali kwa vikundi vya vijana

Kumshauri mkuu wa idara masuala yote yahusuyo maendeleo ya vijana

MIRADI INAYOTEKELEZWA NA IDARA YA MAENDELEO YA JAMII NA MAJUKUMU YA WARATIBU WA MIRADI

KITENGO CHA UKIMWI

Kuhamasisha na kuelimisha jamii juu ya kupunguza kasi ya maambukizi mapya ya UKIMWI

kuratibu mafunzo kwa kamati za kudhibiti UKIMWI za VMAC/WMAC/CMAC

Kutekeleza kazi zote za UKIMWI kama zilivyo kwenye sera ya UKIMWI

Kumshauri mkuu wa idara kuhusu masuala ya UKIMWI

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RUWASA MVOMERO YAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI YA MAJI KWA UFANISI

    April 13, 2025
  • MWENGE WA UHURU KUMULIKA MIRADI YA MAENDELEO 7 YENYE THAMANI YA TSH. 1.06 WILAYANI MVOMRO

    April 13, 2025
  • DC MVOMERO AAGIZA SHULE SHIKIZI MINGO ISAJILIWE, IPOKEE WANAFUNZI JANUARI 2025

    March 27, 2025
  • KUU MVOMERO YAKISHUKURU KIWANDA CHA SUKARI MTIBWA KWA KUSAIDIA WANANCHI KURUDISHA MTO KWENYE MKONDO WAKE

    March 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.