• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

Huduma za Kilimo

1 Sekta ya kilimo

Katika Wilaya ya Mvomero eneo linalofaa kwa kilimo ni Hekta 549, 375, eneo linalolimwa kwa sasa ni Hekta 247,219. Kati ya hizo eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji ni Hekta 77,005, aidha eneo linalomwagiliwa kwa sasa ni Hekta 30,802 (hekta 11,188 miundombinu ya kisasa na hekta 19,614 ni mifereji ya asili). Idadi ya Wakulima ni 172,102 ambao kati yao Wanaume ni 82,115 na Wanawake ni 89,987

1.1 Miundombinu ya Umwagiliaji

Wilaya inaendelea na jitihada za kuboresha miundombinu ya umwagiliaji ya kilimo, hususani ya uboreshaji na ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji. Wilaya inazo skimu za umwagiliaji saba zinazoendelezwa katika hatua tofauti. Skimu hizo ni Dakawa, Kigugu, Hembeti/Dihombo, Lukenge, Mkindo, Ndole na Wami Luhindo. Aidha, miundombinu ya skimu ya Mkindo/Mgongola inaendelea kujengwa kwa usimamizi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC). Kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia 2020/2021 hadi 2022/2023 Wilaya ya Mvomero ilipata jumla ya shilingi 2,698,596,223.50 kutoka kwa Wafadhili mbalimbali wakiwemo Benki ya Dunia, European Union/Helvetas chini ya mradi wa Kuongeza Uzalishaji wa Zao la Mpunga (ERPP) na kupitia mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi Kupitia Mifumo ya Ikolojia Vijijini (EBARR). Fedha hizo zilitumika katika uboreshaji wa miundo mbinu ya umwagiliaji katika skimu ya Kigugu, Hembeti/Dihombo na Lukenge

1.2 Matumizi ya zana bora za kilimo

Wilaya ya Mvomero imeendelea kuwahamasisha Wakulima juu ya matumizi ya zana bora za kilimo, eneo linalolimwa kwa kutumia zana bora za kilimo limeongezeka kutoka asilimia 45 mwaka 2020/2021 hadi asilimia 48 mwaka 2022/2023. Upatikanaji wa zana bora za kilimo umekuwa ukiongezeka kila mwaka.Kwa sasa katika wilaya ya Mvomero kuna jumla ya matrekta makubwa 239, matrekta madogo 87, wanyama kazi 278 na majembe ya wanyama kazi 110.

 1.3 Pembejeo za kilimo

Katika msimu wa mwaka 2023/2024 Wilaya ya Mvomero imeendelea kusajili Wakulima katika madaftari kwa ajili ya kupata namba za siri ili kuweza kununua mbolea za ruzuku. Hadi kufikia Desemba 2023 jumla ya wakulima 27,645 walisajiliwa kwenye madaftari na Wakulima 25,049 walikuwa wamesajiliwa kwenye mfumo na kupata namba za kuwawezesha kununua mbolea za ruzuku.

1.4 Hali ya usalama wa chakula wilayani

Mahitaji ya chakula kwa Wakazi 421,741 wa Wilaya ya Mvomero yanakadiriwa kuwa tani 138,542 (tani 100,058 za chakula aina ya wanga na tani 38,484 za chakula aina ya utomwili). Hali ya upatikanaji wa chakula ni ya kuridhisha katika maeneo yote ya Wilaya ambapo vyakula mbalimbali vinapatikana katika  hifadhi za binafsi za  kaya na  sokoni  kwa bei rafiki.

 1.2  Sekta ya Ushirika

Wilaya ya Mvomero ina jumla vyama vya Ushirika 33 vyenye jumla ya Wanachama 12,753 na vikundi 239. Wanachama hawa na vikundi wana jumla ya hisa zenye thamani ya Tshs. 683,520,000.00 akiba zenye thamani ya Tshs.1,288,208,000.00 na amana zenye thamani ya Tshs. 216,446,000.00

1.2.1  Mikakati ya  kukuza Ushirika 

  1. Kuwahamasisha zaidi Wananchi katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Mvomero waweze kuanzisha Vyama vya Ushirika vya aina mbalimbali kama ilivyofanyika katika maeneo ya Kinda na Kweuma ambapo Chama cha Ushirika cha Wakulima wa zao la Kahawa (KINDA AMCOS) na Chama cha Ushirika cha wakulima wa Kakao (URAFIKI AMCOS) vimeshasajiliwa. Pia Wakulima wa Kahawa wa Kata za Maskati na Wakulima wa Kata ya Mziha, Sungaji na Diongoya wapo katika hatua mbali mbali za uhamasishaji na baadhi yao kuandaa Masharti kwa ajili ya zoezi la usajili.
  2. Kuendelea kuimarisha utaratibu wa kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani ili Wakulima waweze kutumia mfumo huu unaosimamiwa na soko la bidhaa la Tanzania (TMX) na hatimaye kuuza mazao ya kimkakati katika mfumo huo
  3. Kuwajengea uwezo Watendaji wa Vyama vya Ushirika kwa Kutoa mafunzo wakati wa kazi kwa Mameneja/Makatibu na Wahasibu/Makarani na Maafisa mikopo wa vyama hivyo.
  4. Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa hesabu za vyama vya Ushirika na uchunguzi ili kubaini kasoro zinazojitokeza.

1.2.2 Mafanikio katika sekta ya Ushirika

  1. Katika msimu wa kilimo 2021/2022 Wakulima wa Kata za Mangae na Mziha wamefanikiwa kuuza ufuta wao kupitia mfumo wa Stakabadhi Ghalani ambapo na kupata Tshs. 15,275,000.00 kwa kuuza tani 9.40 za ufuta na Wilaya  kupata ushuru kupitia TMX kiasi cha Tshs. 526,400.00
  1. Wakulima wa Mhonda na Kwema wamefanikiwa kuuza kakao yao kupitia mfumo wa Stakabadhi Ghalani ambapo na kupata Tshs. 10,486,808,447.00 kwa kuuza tani 1,627,579 za Kakao na Wilaya  kupata ushuru kupitia TMX kiasi Tshs. 238,330,574.00 
  2. Wakulima kutolanguliwa kwani wanapata bei ya moja kwa moja kutoka kwa mnunuzi na bei watakayokubaliana ndiyo wanayolipwa bila kuingia gharama yoyote ya kupunjwa kwa kutumia vipimo visivyokuwa rasmi.
  1. Mikopo yenye thamani ya Tshs. Tshs. 1,478,817,750.00  imetolewa kwa Wanachama wa Vyama vya Ushirika wa Akiba na mikopo hai 8 vya Wilaya ya Mvomero kwa kipindi cha Juni 2022.

Chama cha Ushirika cha Wakulima wa miwa cha Turiani (TUCOCPRCOS LTD) kimewezeshwa kupatiwa Mkopo wenye thamani ya Tshs.220, 000,000/=  ili kununua mashine ya kuvunia miwa (Kameko-Cane loader) kutoka benki ya EFTA na tayari mkopo huo umekwisha rejeshwa.

Kushirikiana kwa ukaribu na vyombo vingine vya Dola kama vile TAKUKURU na Mahakama kuwabana wabadhirifu katika Vyama vya Ushirika na kufanikiwa kurejesha pesa za Chama kiasi cha 123,924,000/= kati ya 461,000,000/= zilizochukuliwa katika Chama cha Akiba na Mikopo cha TURSACCOS kilichopo Turiani. Kiasi kilichobakia kinaendelea kufuatiliwa ili nacho pia kirejeshwe na hatimaye wanachama wafaidike na fedha zao kupitia mikopo.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RUWASA MVOMERO YAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI YA MAJI KWA UFANISI

    April 13, 2025
  • MWENGE WA UHURU KUMULIKA MIRADI YA MAENDELEO 7 YENYE THAMANI YA TSH. 1.06 WILAYANI MVOMRO

    April 13, 2025
  • DC MVOMERO AAGIZA SHULE SHIKIZI MINGO ISAJILIWE, IPOKEE WANAFUNZI JANUARI 2025

    March 27, 2025
  • KUU MVOMERO YAKISHUKURU KIWANDA CHA SUKARI MTIBWA KWA KUSAIDIA WANANCHI KURUDISHA MTO KWENYE MKONDO WAKE

    March 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.