• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

Huduma za Afya

1  Huduma za Afya Hospitali, Vituo vya Afya na Zahanati)

Idara ya Afya inatoa huduma za afya ya tiba na kinga. Upande wa afya kinga kuna huduma za afya ya uzazi na mtoto,usafi wa mazingira, UKIMWI,kifua kikuu na ukoma,Malaria na huduma za afya shuleni.Wilaya ya Mvomero ina jumla vituo vya kutolea huduma za afy 83.ikiwa na hospitali 3 vituo vya afya 10 na zahanati 70

Jedwali Na.16:  Idadi ya hospitali, vituo vya afya na zahanati

JINA LA KITUO
SERIKALI
MASHIRIKA YA DINI
BINAFSI
JUMLA
Hospitali
1
1
1
3
Vituo vya afya
8
2
0
10
Zahanati
57
7
6
70
JUMLA
66
10
7
83

7.2 Hali ya Watumishi

Sekta ya afya ina mahitaji ya watumishi 1052 wa kada mbalimbali, mpaka sasa kuna watumishi   519 na hivyo kufanya upungufu wa watumishi 533

7.3  Miradi ya maendeleo (miundombinu) iliyotekelezwa katika kipindi cha kuanzia Julai 2021 hadi  Desemba  2023

Katika kipindi cha kuanzia mwaka wa fedha Julai 2021 hadi Desemba 2023 Wilaya ya Mvomero  imefanikiwa kutekeleza miradi mbalimbali ya ujenzi wa miundombinu katika sekta ya afya. Jumla ya kiasi cha Tsh 3,073,000,000.00 zimetolewa kwenye ujenzi wa miundombinu ya afya na jumla ya majengo 28 yamejengwa  kama inavyoonekana kwenye jedwali Na.17  hapa chini.

Jedwali Na 17:  Miradi ya Maendeleo (Miundombinu) iliyotekelezwa katika Sekta ya Afya

Jina la mradi
Aina ya majengo yaliyojengwa
Idadi ya majengo yaliyojengwa
Kiasi cha fedha kilichotolewa
Ujenzi wa hospitali ya Wilaya
  1. Jengo la wagonjwa wa dharula
  2. Wodi za wanawake 2
  3. Wodi ya wanaume
  4. Jengo la upasuaji
  5. Nyumba ya mtumishi
  6. Kichomea taka
  7. Walk ways
7
1,440,000,000
Ujenzi wa kituo cha afya Mziha
  1. Jengo la wagonjwa wan je
  2. Jengo la wazazi
  3. Jengo la upasuaji
  4. Maabara
  5. Jengo la kufulia
  6. Kichomea taka
6
500,000,000
Ujenzi wa kituo cha afya Dakawa
1.Jengo la wagonjwa wa nje
2.Jengo la maabara
3.Kichomea taka
3
275,000,000
Uboreshaji wa kituo cha afya Mlali
1.Jengo la upasuaji
2. Jengo la wazazi
3.Jengo la maabara
4.Nyumba ya watumishi
5.Jengo la kuhifadhia maiti
6.Kichomea taka
6
558,000,000
Ukamilishaji ujenzi wa zahanati 6 za Kidudwe,Manyinga, Misengele,Difinga,Tchenzema na Ndole
Zahanati
6
300,000,000
JUMLA
 
 
3,073,000,000

 

7.4 Mfuko wa Afya ya Jamii iliyoboreshwa (ICHF)

Mfuko wa Afya ya Jamii CHF iliyoboreshwa ilizinduliwa tarehe 1/7/2019 katika halmashauri ya wilaya ya Mvomero , kama ilivyo katika Mwongozo kila kaya yenye watu 6 hujiunga kwa Tshs 30,000/=  kwa ajili ya kupata huduma za afya kwa mwaka mzima.Hadi kufikia Desemba 2023 ,jumla ya kaya 16,410   zimejiunga na mfuko wa CHF kati ya kaya  72,519  zilizopo Wilayani Mvomero. Idadi hii ya kaya ni sawa na  asilimia  23 ya kaya zote zinazotakiwa kujiunga na mfuko wa Ichf.  Aidha kiasi cha fedha iliyokusanya katika huu mfuko katika hiki kipindi  ni Tshs 93,390,000.00

7.5 Mfumo wa Serikali  wa taarifa za wagonjwa na ukusanyaji  wa mapato (Got-homis)

Hadi kufikia Oktoba 2023 mfumo wa Got-homis umefungwa katika vituo vya kutolea huduma za afya 13 na unafanya kazi. Vituo hivyo ni Hospitali ya wilaya,Kituo cha afya Mvomero,Kituo cha afya Kibati, Kituo cha afya Mgeta, Kituo cha afya Mlali,Kituo cha afya Melela, zahanati ya Lusanga, zahanati ya Milama, zahanati ya Nyandira,zahanati ya Mkindo

7.6 Msamaha ya wagonjwa.

Makundi ya Wagonjwa wa Msamaha  ni kina mama wajawazito,watoto chini ya miaka 5, magonjwa sugu, wazee na walemavu.  Katika kipindi cha kuanzia Julai 2021 hadi kufikia Desemba  2023, thamani  ya fedha zilizotolewa msamaha kwa makundi haya ya wagonjwa ni kiasi cha Tsh 289,368,000.00

7.7 Hali ya upatikanaji wa dawa

Hali ya upatikanaji wa dawa ni ya kuridhisha, mpaka kufikia Desemba 2023 upatikanaji wa dawa na vifaa tiba ilikuwa ni  92% na upatikanaji wa dawa za msingi  ilikuwa 95 % .

  • 7.8  Hali ya Afya ya  Uzazi na Watoto

Huduma ya baba, mama na mtoto inatolewa katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma za Afya Wilayani. Huduma zinazotolewa ni pamoja na:-

  • Huduma kwa wajawazito
  • Huduma ya uzazi kwa njia ya kawaida na upasuaji
  • Huduma ya uzazi baada ya kujifungua kwa mama na mtoto
  • Upimaji wa saratani ya matiti na mlango wa kizazi
  • Huduma ya ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto
  • Huduma za uzazi wa mpango kwa baba na mama
  • Huduma ya kujikinga na magonjwa ya kuambukiza hasa yanayozuilika kwa chanjo
  • Huduma ya mkoba ya chanjo na uzazi wa mpango

7.8.1 Mafanikio ya utoaji huduma ya afya ya uzazi na mtoto wilayani  kwa kipindi cha Julai  2021 hadi  Desemba  2023

  • Kuongezeka kwa vituo vya huduma ya uzazi salama na huduma ya upasuaji wa dharula kutoka vituo 5 hadi vituo 10
  • Kuongezeka kwa akina mama wanaojifungulia kwenye vituo vya kutolea huduma kutoka 9807 hadi kufikia 22,474
  • Kupungua kwa vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi  kutoka vifo 17 mwaka 2021 hadi vifo 8 mwaka 2023
  • Kupungua kwa vifo vya watoto tumboni kutoka vifo 107 mwaka 2021 hadi kufikia vifo 83 mwaka 2023
  • Kuongezeka kwa watoto wanaopata huduma za chanjo kutoka watoto 26,730(80.5%) mwaka 2021 hadi kufikia watoto 35,430(99.5)

 7.9 Magonjwa ya mlipuko

Katika kipindi cha kuanzia  Julai 2021  Oktoba 2023 jumla ya wagonjwa 53 walihisiwa kuwa na ugonjwa wa surua katika vijiji vya Mkindo na Wami Dakawa.Ufuatiliaji ulifanyika na hatua za kuzuaia maambuzi kuendelea kuenea zilichukuliwa

7.9.1 Mikakati ya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko

Katika kukabiliana na magonjwa ya mlipuko Halmashauri inaendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya kujikinga na kuzuia milipuko kwa kuzingatia kanuni za afya kupitia mbinu shirikishi (Community led total sanitation). Aidha, kuna utoaji wa chanjo mbalimbali kwa watoto na akina mama kwenye vituo vya kutolea huduma, kuzuia  magonjwa ya mlipuko mfano surua

7.10  Hali ya maambukizi ya VVU na UKIMWI Wilayani Mvomero

Kiwango cha maambukizi ya virusi vya Ukimwi Wilayani bado ni kikubwa.  Wilaya  kwa kushirikiana na wadau wake wa maendeleo inaendelea kuelimisha jamii jinsi ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Ukimwi hasa vijana na kutoa huduma kwa walioathirika na VVU.  Wilaya ya Mvomero  inavyo vituo  83 vya utoaji wa dawa dhidi ya virusi  geuzi (hospiali  3 vituo vya afya 10  na zahanati 70  

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RUWASA MVOMERO YAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI YA MAJI KWA UFANISI

    April 13, 2025
  • MWENGE WA UHURU KUMULIKA MIRADI YA MAENDELEO 7 YENYE THAMANI YA TSH. 1.06 WILAYANI MVOMRO

    April 13, 2025
  • DC MVOMERO AAGIZA SHULE SHIKIZI MINGO ISAJILIWE, IPOKEE WANAFUNZI JANUARI 2025

    March 27, 2025
  • KUU MVOMERO YAKISHUKURU KIWANDA CHA SUKARI MTIBWA KWA KUSAIDIA WANANCHI KURUDISHA MTO KWENYE MKONDO WAKE

    March 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.