• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

Posted on: August 20th, 2025

Wilaya ya Mvomero imeweka mikakati madhubuti ya kuboresha usafi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuinua afya ya jamii na kuongeza nafasi ya wilaya hiyo kufanya vizuri katika tathmini ya kitaifa ya usafi wa mazingira.

Hayo yamebainishwa Agosti 20, 2025 wakati wa kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi ngazi ya Wilaya kilicholenga kujadili utekelezaji wa kazi mbalimbali za Divisheni ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe mwaka 2022 - 2025, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.

Akizungumza wakati wa kufunguka kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Maulid Dotto amesema kuwa usafi wa mazingira ni ajenda ya kipaumbele, hasa ikizingatiwa kuwa mazingira machafu yanachangia kwa kiasi kikubwa milipuko ya magonjwa kama kipindupindu, homa ya matumbo na malaria.

Aidha, Mhe. Maulid Dotto ameongeza kuwa kama Wilaya inatakiwa kuwa na mikakati madhubuti ya kuhakikisha kuwa inafanya vizuri kwenye kipengele cha usafi wa mazingira huku akitaja baadhi ya mikakati itakayosaidia kufikia lengo hilo.


"...tuongeze juhudi za kuhakikisha tunashinda katika mashindano tunayoshiriki yanayohusu usafi wa mazingira...lakini pia tuwe na lengo letu kama wilaya na kwa mwaka huu tumekubaliana kwamba tunatoka kwenye namba 83 tushike namba 50..." amesema Mkuu wa Wilaya.


Baadhi ya mikakati iliyoahinishwa na Mkuu wa Wilaya ni pamoja na kuanzisha siku maalum ya usafi wa mazingira ambayo italenga kuhimiza usafi, kufanya ziara za kushtukiza kwenye maeneo mbalimbali Wilayani humo, Mashindano ya usafi baina ya vijiji, kata, shule na masoko, ambapo washindi watapewa zawadi na kutangazwa hadharani.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Ndg. Paulo Faty amesema kuwa kwa mashindano ya mwaka huu Halmashauri imeweka lengo la kushika nafasi ya 50 akiahidi kuwa lengo hilo litafikiwa.


Naye, Afisa Afya wa Wilaya hiyo Bw. Morgan Towo ameeleza kuwa baadhi ya maeneo bado yana changamoto ya watu kujisaidia porini, ukosefu wa vyoo vya kisasa na uhifadhi hafifu wa taka za majumbani na masokoni, mikakati imewekwa kuhakikisha inabadilika.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.