Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mhe. Maulid Dotto, amelipongeza Shirika la SAWA WANAWAKE TANZANIA kwa jitihada zake za kuchangia maendeleo ya sekta ya elimu wilayani humo kupitia ujenzi wa madarasa ya shule shikizi katika eneo la Kwa Wagogo hatua hiyo itasaidia kupunguza changamoto ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kupata elimu



Mhe. Maulid Dotto ametoa pongezi hizo Januari 23, 2026 wakati wa hafla ya kupokea mradi huo uliojengwa kwa ushirikiano wa Shirika la SAWA pamoja na wananchi wa eneo hilo.
Mkuu huyo wa Wilaya amesema ujenzi wa miundombinu hiyo ni mfano wa ushirikiano mzuri kati ya Serikali na wadau wa maendeleo, akisisitiza kuwa shirika hilo limekuwa la kizalendo kwa kutatua changamoto za watoto wa kitanzania ambao wamekuwa wakipata adha ya kupata elimu.




Aidha, amemuagiza mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kuhakikisha mchakato wa usajili wa shule hiyo unaanza mara moja ili kuwezesha watoto kuanza masomo kwa wakati, sambamba na kukamilisha taratibu zote za kisheria na kiutawala.



Sambamba na hilo, Mkuu wa Wilaya amewahimiza wananchi wa eneo hilo kuendelea kujitoa kuchangia ujenzi wa madarasa mengine ili shule hiyo iweze kujitegemea kama shule nyingine na kutunza miundombinu hiyo ili iweze kudumu. Pia, amesitiza kuwa Serikali ya Wilaya itaendelea kutoa ushirikiano wa karibu kwa Shirika la SAWA na wadau wengine ili kuhakikisha miradi ya elimu inatekelezwa kwa ubora na kwa kuzingatia malengo ya Serikali ya kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia kwa watoto wote.

Naye, Mkurugenzi wa Shirika hilo, Bi. Helen Mkalang'ambo ameushukuru uongozi wa Wilaya ya Mvomero kwa ushirikiano wanaoupata wakati wa kutekeleza miradi yao, huku akibainisha kuwa mradi huo umehusisha ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa, ofisi pamoja na matundu vya vyoo, aidha, shirika limekamilisha ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa ambavyo vimejengwa kwa nguvu ya wananchi.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Dakawa Mhe. Joshua Lugaso amemshukuru Mkurugenzi wa shirika hilo pamoja na wananchi wa eneo hilo la Kwa wagogo kwa ushirikiano wao hadi kufanikisha

Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero
Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO
Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348
Mobile: +255 23 293 4348
Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz
Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.