Viongozi wa vijiji wametakiwa kusimama imara na kuhakikisha kuwa fursa za uwekezaji na maendeleo hazigeuki kuwa chanzo cha migogoro ya mipaka baina ya vijiji, bali zinatumika kama kichocheo cha ustawi wa wananchi na maendeleo endelevu.

Wito huo umetolewa Januari 28, 2026 na Katibu Tawala Wilaya ya Mvomero Ndg. Said Nguya alipotembelea Kata ya Melela kusuluhisha mgogoro wa mpaka kati ya Kijiji cha Melela na Magali.
Katibu Tawala huyo ameeleza kuwa migogoro mingi ya mipaka inachochewa na kuibuka kwa fursa za kiuchumi ikiwemo uwekezaji katika Sekta za madini, minala ya mawasiliano pamoja na miradi mbalimbali ya maendeleo, hali inayosababisha migongano ya maslahi endapo mipaka haijawekwa wazi na kusimamiwa ipasavyo.


Aidha, Ndg. Nguya wamewataka wenyeviti wa vijiji, watendaji wa vijiji na wajumbe wa halmashauri za vijiji kuukubali ukweli pindi migogoro hiyo inaposuluhishwa pamoja na kuzingatia misingi ya sheria, taratibu na uwazi katika usimamizi wa ardhi na rasilimali.




Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero
Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO
Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348
Mobile: +255 23 293 4348
Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz
Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.