• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MAMLAKA ZA UDHIBITI ZISHIRIKISWE KWENYE MAONESHO YA NANE NANE KUWASAIDIA WAJASIRIAMALI WADOGO KUONGEZA THAMANI KWENYE BIDHAA ZAO

Posted on: August 2nd, 2025

Wito umetolewa kwa waandaaji wa Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki kushirikisha kikamilifu mamlaka za udhibiti wa ubora kama TBS, TMDA, TFDA na WMA ili kuwasaidia wajasiriamali wadogo kuongeza thamani kwenye bidhaa wanazozalisha na hivyo kuweza kushindana katika soko la ndani na nje ya nchi.

Wito huo umetolewa Agosti 2, 2025 na Mhe. Mizengo Kayanza Pinda Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Nane nane Kanda ya Mashariki 2025 ambayo yanafanyika katika viwanja vya Mwl. J. K. Nyerere vilivyopo katika Manispaa ya Morogoro.

Mhe. Pinda amesema kuwa lengo la kuwashirikisha mamlaka hizo kuona namna wajasiliamali hao wanavyozalisha bidhaa zao na kuwasaidia kuongeza thamani katika bidhaa hizo ili kurahisisha katika upatikanaji wa masoko ya uhakika.


“…wakati wa maonesho kama haya tuombe mamlaka zile ambazo zimepewa jukumu la kusimamia ubora wa bidhaa mbalimbali tuzifanye kuwa sehemu ya Mikoa ya Kanda hii ya Mashariki…” amesema Mhe. Pinda.


Aidha, Waziri Mkuu huyo Mstaafu amewapongeza Wajasiliamali wa Kanda ya Mashariki kwa kuendelea kuboresha bidhaa zao hali inayowaongezea uhakika wa masoko.


Naye, Mkuu wa Mkoa wa Pwani na Mwenyekiti wa Maonesho hayo 2025 Mhe. Abubakar Kunenge amesema kuwa maonesho ya mwaka huu yanalenga kuonesha kwa vitendo mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, huku akitoa rai kwa wananchi kutembelea katika maonesho hayo ili waweze kujifunza mbinu na Teknolojia za kisasa za Kilimo, Ufugaji na Uvuvi.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amebainisha kuwa kwa mwaka huu wakulima, wafugaji, wavuvi pamoaja na Wananchi watapata elimu ya biashara kuhusiana na shughuli zao kwenye banda maalum la B2B yaani Business to Business. Banda hilo litakuwa na wataalam wa kutoa mafunzo kwa wananchi ambayo itawasaidia kuongeza tija katika kilimo, ufugaji na uvuvi.


Maonesho ya Nane nane Kanda ya Mashariki yalianza Agosti 1 na yatahitimishwa Agosti 8.


MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.