• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

ZAIDI YA MILIONI 670 ZIMETOLEWA KWA VIKUNDI 79, DC MVOMERO ATOA AGIZO FEDHA ZITOLEWE KWA WAKATI

Posted on: January 10th, 2025

Zaidi ya shilingi milioni 679 zimetolewa kwa vikundi 79 vya wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu wilayani Mvomero, ikiwa ni sehemu ya mpango wa serikali wa kuwezesha wananchi kiuchumi.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa utoaji mikopo hiyo Wilayani Mvomero iliyofanyika leo Januari 10, 2024 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri, Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Judith Nguli amemuagiza Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kuhakikisha kuwa hadi kufikia siku ya jumatano ya Wiki ijayo vikundi hivyo vinapata fedha hizo ili viendelee na shughuli za uzalishaji. 

“...kuhakiki tu unaweza kutumia jumamosi, jumapili, jumatatu...ikifika jumatano sisi tunacheka...” amesisitiza Mkuu wa Wilaya.

Aidha, Mhe. Nguli amewaagiza Maafisa ugani wa Kata, Maafisa biashara, maafisa maendeleo ya jamii pamoja na watendaji wa Vijiji na Kata kuhakikisha kuwa wanavisimamia vikundi hivyo pamoja na kuwapatia elimu juu ya miradi wanayobuni ili fedha zilizotolewa zilete tija.

Hata hivyo, Mkuu huyo wa Wilaya amewaonya wanufaika dhidi ya matumizi mabaya ya mikopo hiyo, akiwahimiza wawekeze katika miradi yenye tija kama kilimo, ufugaji, na biashara ndogo ndogo ili kuboresha maisha yao na kuchangia maendeleo ya wilaya.

Naye Mbunge wa Jimbo la Mvomero Mhe. Jonas Van Zeeland amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu Halmashauri zote hapa nchini kutoa mikopo hiyo. Aidha, Mbunge ameushukuru uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kwa kutenga fedha za asilimia 10 kutoka kwenye Makusanyo yake kwa ajili ya kuwainua wananachi kiuchumi.

Awali akitoa taarifa ya tathmini ya vikundi vilivyoomba mikopo hiyo, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Bw. Mashaka Malole amesema jumla ya vikundi vya wanawake 57 vinatarajia kupata kiasi cha shilingi milioni 428.4, vikundi vya vijana 17 watapata shilingi milioni 218.5 na vikundi vya wenye ulemavu ni vinne ambavyo vitapata shilingi milioni 24.

Kwa upande wao baadhi ya wanufaika wa mikopo hiyo akiwemo Bi. Jackline Mwaisiga mkazi wa Kata ya Mzumbe akiwakilisha kundi la watu wenye ulemavu amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kulikumbuka kundi hilo la wenye ulemavu, akisema kuwa kupitia mikopo hiyo itawawezesha kujiinua kiuchumi na kushiriki katika fursa ambazo awali walikuwa hawashiriki.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.