• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WIZARA YA KILIMO YATAKIWA KUVUNJA MKATABA WA UKARABATI SKIMU YA UMWAGILIAJI MGONGOLA, MKANDARASI ATAKIWA KULIPA FIDIA.

Posted on: February 16th, 2025

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeielekeza Wizara ya Kilimo kuvunja mkataba wa ukarabati wa Skimu ya Umwagiliaji ya Mgongola iliyopo katika Kata ya Mkindo kutokana na kutoridhishwa na utekelezaji wake.

Hatua hiyo imekuja baada ya kamati hiyo kufanya ukaguzi Februari 16, 2025 kwenye mradi huo na kubaini dosari mbalimbali, zikiwemo mkandarasi kushindwa kutimiza masharti ya mkataba ikiwemo kukamilisha mradi kwa wakati.

Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Mariamu Ditopile Mzuzuri amesema kuwa licha ya serikali kutenga fedha kiasi cha shilingi Bilioni 5.6 kwa ajili ya kuimarisha skimu hiyo, utekelezaji wake umekuwa wa kusuasua.

"...huu mkataba kwanza umeshaisha kwahiyo kwa mujibu wa sheria uende ukavunjwe na kama kuna hasara yoyote imeenda aidha kwa Serikali  ama kwa wananchi iende ikalipwe ipasavyo na huyu mkandarasi..." amesema Mhe. Mzuzuri.

Aidha, Kamati hiyo imemtaka Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya umwagiliaji kufika mara moja katika mradi huo ili kuangalia mradi pamoja na kufanya maboresho katika mkataba mpya kama utasainiwa kuhakikisha kuwa eneo la uzalishaji linaongezeka kufikia hekta 1500 pamoja na marekebisho ya chanzo cha maji  ili kuongeza uwezo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema lengo la Mkoa ni kuifanya skimu hiyo kuwa ya mfano wa kilimo cha mpunga nchini kwa kufanya maboresho ya chanzo ili kuongeza eneo la uzalishaji wa kilimo shadidi kutoka hekta 620 hadi hekta 1500 na kukaribisha wawekezaji kwenye hekta 1500 zilizobaki kuendelea kuongeza uzalishaji.

Naye Mbunge wa Jimbo la Mvomero Mhe. Jonas Van Zeeland ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kwa kutoa fedha zaidi ya shilingi bilioni 5.6 kwa ajili ya skimu hiyo.

Awali akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo Mhandisi wa Umwagiliaji Mkoa wa Morogoro kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Mhandisi Juma Mattanga amebainisha kuwa mkandarasi alianza kazi tarehe 7 Septemba, 2022 na muda wa kukamilisha mradi ilipaswa kuwa tarehe 6 Septemba, 2023 lakini mkandarasi aliongezewa siku 120 hivyo ulitakiwa kukamilika tarehe 6 Januari, 2024 hadi sasa mradi huo upo asilimia 44 ya utekelezaji na kazi imesimama.

MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.