• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DC MVOMERO ATOA SIKU SABA WAFUGAJI WALIOVAMIA SKIMU YA UWAWAKUDA KUONDOLEWA

Posted on: December 17th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Maulid Dotto ametoa siku saba kwa Wenyeviti na Watendaji wa Vijiji vyote vya Kata ya Dakawa kwa kushirikiana na Viongozi wa chama cha wafugaji na viongozi wa kimila wa jamii ya kifugaji kuhakikisha kuwa wanaondoa na kuzuia mifugo yote inayoingia katika skimu umwagiliaji ya Ushirika wa Wakulima Wadogo wadogo wa mpunga Dakawa (UWAWAKUDA) kuanzia Disemba 17 hadi 24, 2025.


Mhe. Dotto ametoa agizo hilo Disemba 17 wakati wa kikao cha wadau wa UWAWAKUDA ambacho kimefanyika katika Ofisi za ushirika huo, kabla ya kikao hicho Mkuu huyo wa Wilaya ametembelea na kukagua eneo la shamba hilo na kujionea uharibifu wa miundombinu uliyofanywa na mifugo.


Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mkuu huyo wa Wilaya amesema uvamizi wa wafugaji umesababisha uharibifu wa miundombinu, migogoro kati ya wakulima na wafugaji, pamoja na kupunguza tija ya uzalishaji wa mazao.


Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi wa Skimu hiyo Bw. Nasibu Katoto amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa agizo hilo huku akisisitiza kuwa kila mtendaji kwa nafasi yake asimamie sheria na kutekeleza wajibu wake ipasavvyo.


Kwa upande wake, Meneja wa UWAWAKUDA Bi. Irene Calist ameeleza kuwa uwepo wa mifugo katika eneo hilo umekuwa ukisababisha uharibifu wa mifereji ya maji, mashamba ya wakulima na kusababishia harasa kwani hutumia zaidi ya milioni 300 kila mwaka kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu hiyo.


Aidha, amebainisha kuwa Serikali kupitia Wizara ya Kilimo ilitoa kiasi cha shilingi bilioni 24 kwa ajili wa ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji ambapo uzalishaji uliongezeka kutoka gunia 10 hadi gunia 40 kwa hekta.


Diwani wa Kata ya Dakawa Mhe. Joshwa Makukula ameushauri uongozi wa skimu hiyo kushirikisha viongozi wa Vijiji katika kamati zao za ulinzi na usalama ili kuongeza nguvu katika ulinzi wa shamba hilo, pia amewataka kuona namna ya kukusanya masalia ya majani na kuyahifadhi na kuyauza kwa wafugaji husasan kipindi cha kiangazi na kwamba itasaidia kuondoa adha hiyo.



MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC DOTTO AZUIA ENEO LA KIJIJI LILILOUZWA KINYUME NA UTARATIBU, AAGIZA ALIYENUNUA ARUDISHIWE FEDHA ZAKE

    December 18, 2025
  • AHADI YA RAIS SAMIA KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE YAANZA KUTEKELEZWA, WASIMAMIZI VITUO VYA AFYA WAJENGEWA UWEZO KUFANIKISHA

    December 18, 2025
  • DC MVOMERO ATOA SIKU SABA WAFUGAJI WALIOVAMIA SKIMU YA UWAWAKUDA KUONDOLEWA

    December 17, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA: WANANCHI WAPATA GARI LA WAGONJWA, WAISHUKURU SERIKALI KUWAONDOLEA ADHA KUSAFIRISHA WAGONJWA WA RUFAA

    December 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.