Wananchi wa Kata ya Mziha, Wilaya ya Mvomero, wameandika historia mpya baada ya kupokea gari la wagonjwa (Ambulance) lililotolewa na Serikali, hatua inayokwenda kuwaondolea adha kubwa ya usafirishaji wa wagonjwa wanaohitaji rufaa kwenda vituo vya afya vya ngazi ya juu.
Akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi gari hilo, Diwani wa Kata hiyo Mhe. Denis Ezekiel amesema upatikanaji wa gari hilo utaboresha kwa kiasi kikubwa huduma za afya, hasa katika nyakati za dharura ambapo awali walilazimika kuazima gari la wagonjwa kutoka katika kituo cha Afya cha Chazi akiongeza kuwa wakati mwingine gari hilo halikupatikana.
“…kwa kweli hii adha ilikuwa ni kubwa sana tulikuwa tunapata ambulance kutoka Chazi, usiku wa manane tunapiga simu mara nyingine haipatikani lakini leo tunaandika historia mpya yam waka huu kwamba tumepewa ambulance ambayo imeandikwa Kata ya Mziha…” amesema Mhe. Diwani.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kijiji cha Mziha Bw. Rajab Bakari kwa niaba ya wananchi wa Mziha ameishukuru Serikali kwa kusikiliza kilio chao na kuchukua hatua Madhubuti, huku akibainisha kuwa walilazimika kutumia pikipiki kusafirisha wagonjwa, jambo lililoongeza mzigo wa gharama kwa familia maskini. Ameongeza kuwa gari hilo litasaidia kupunguza vifo vya akinamama wajawazito na watoto wachanga ambao wamekuwa katika hatari kubwa ya kupoteza Maisha.
Akizungumza wakati akikabidhi gari hilo kwa wananchi wa Kata hiyo, Mbunge wa Jimbo la Mvomero Mhe. Sarah Msafiri Ally amewataka wasimamizi wa gari hilo kuhakikisha kuwa linatoa huduma iliyokusudiwa na kwamba kila mwananchi ana haki ya kulitumia gari hilo.
Aidha, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho pamoja na fedha za utekelezaji wa mradi wa maji utakao wahudumia wananchi wa Kata hiyo.
Akitoa taarifa ya ujenzi wa kituo hicho, Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Alex Mzava amebainisha kuwa Serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 500 ikiwa ni fedha za tozo ambapo imetumika kujenga jengo la wagonjwa wa nje (OPD), Maabar
Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero
Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO
Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348
Mobile: +255 23 293 4348
Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz
Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.