• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WILAYA YA MVOMERO YAPATA UGENI KUTOKA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR

Posted on: March 9th, 2024

Machi 09, 2024 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero imepokea ugeni kutoka Baraza la Wawakilishi likiongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Harusi Said Suleiman na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi inayoongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Machano Othman Said pamoja na Kamati ya Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais katika ziara ya ukaguzi wa mradi wa kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia Mfumo wa Ikolojia Vijijini (EBBAR) uliopo katika Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro.

Waziri Harusi amekagua mradi wa lambo kwa ajili ya kuvunia maji lenye thamani ya Sh. 293,654,565.32 ambalo linatumika kumwagilia ekati 4 za zao la nyanya kwa kutumia mfumo wa umwagiliaji wa matone, pia bwawa hilo linanufaisha wananchi kwa uwepo wa samaki aina ya sato ambao wamepandikizwa katika bwawa hilo.

Pia amekagua ujenzi wa kiwanda cha kuchakata bidhaa za ngozi wenye thamani ya Sh. 108,010,000.00 ambao utanufaisha vijana kwa kujiajiri na mradi wa shamba la uzalishaji uyoga wenye thamani ya Sh. 5,500,000 katika Kijiji cha Melela kata ya Melela.

Waziri huyo na Kamati ya Wajumbe wa Baraza pia walitembelea katika Kijiji cha Mingo kilihopo Kata ya Lubungo na kukagua mradi wa kisima kirefu cha umwagiliaji wa mazao ya mbogamboga kwa kutumia umeme wa nguvu za jua (Solar) wenye thamani ya Sh. Milioni 22.

Waziri amesema “...mradi huo umewapatia wananchi wa Wilaya ya Mvomero manufaa makubwa kwa kuweza kupata ajira ambayo inawasaidia katika kuendesha maisha yao ya kila siku”.

Aidha amewataka wasimamizi wa mradi huo kuendelea kuutunza na kuudumisha ili uendelee kuleta manufaa zaidi kwa wananchi na kuwarahisishia kupata huduma za kijamii zikiwemo maji yanayowasaidia katika shughuli za kilimo na ufugaji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Ofisi ya kusimamia Ofisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi Mhe. Machano Othmani Said amesema mradi huo utawasaidia wananchi kujikwamua na umaskini na kuwarahisishia kupata huduma za kijamii kwa urahisi, hivyo amewataka wananchi kuitunza miradi hiyo ili iweze kudumu na kuwasaidia kujipatia kipato na huduma za jamii hususan maji kutokana na uwepo wa visima na malambo yaliyopo katika maeneo hayo.

Mhe. Machano amewataka wananchi waendelee kuthamini mchango wa Serikali zote mbili (Muungano) katika kuleta maendeleo kwa wananchi wake.

Wilaya ya Mvomero ni moja kati ya Wilaya zinazotekeleza mradi wa Kukabiliana na mabadiliko ya Tabia Nchi kwa Kutumia Mifumo ya Ikolojia Vijijini (EBBAR), mradi huu unafadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia (GEF). Wilaya nyingine zinazotekeleza mradi huu Tanzania Bara ni Mpwapwa (Dodoma), Simanjiro (Manyara) na Kishapu (Shinyanga) kwa upande wa Zanzibar ni Matemwe (Unguja).

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.