Waandaaji wa maudhui mtandaoni katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero wamejitokeza kuchukua fomu za usajili ili waweze kutambulika na kupata fursa za mikopo zilizotangazwa na Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Makonda.

Akitangaza fursa hiyo Januari 30, 2026 jijini Dodoma Mhe. Makonda amesema Wizara hiyo imepatiwa kiasi cha Sh. Bilioni 2 itakayowawezesha watengeneza maudhui mitandaoni kuimarisha kazi zao na kuwaongezea kipato kupitia majukwaa ya kidigitali.


Wakiongea baada ya kukabidhiwa fomu za usajili na Afisa Mawasiliano Serikalini wa Halmashauri, waandaaji hao wameishukuru Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwasajili na kuwatambua na kushauri watengeneza maudhui wachangamkie fursa hii wajitokeze kuchukua fomu ili waweze kuboresha kazi zao.


Zoezi la uchukuaji wa fomu limeanza Januari 30, 2026 na litakamilika Februari 15, 2026, ambapo watengeneza maudhui wanatakiwa kufika Ofisi za Halmashauri Kitengo cha Mawasiliano Serikali zikiainisha taarifa binafsi na shughuli wanazofanya.
MWISHO
Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero
Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO
Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348
Mobile: +255 23 293 4348
Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz
Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.