Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe (Mb) amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini, akisema hatua hiyo imeleta chachu kubwa ya kuboresha huduma za kijamii na kuchochea maendeleo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Prof. Shemdoe ameyasema hayo Januari 17, 2026 katika kikao ambacho kimewakutanisha Viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Morogoro akiwemo Mkuu wa Mkoa huo, Katibu Tawala Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Makatibu Tawala wasaidizi, Wenyeviti wa Halmashauri, pamoja na Wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri za Mkoa wa Morogoro katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa ya Morogoro



Waziri huyo amesema Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo inawagusa moja kwa moja wananchi wake akitolea mfano fedha zaidi ya Tsh. Bilioni 30 zimetolewa kwa ajili ya mradi wa barabara, kituo cha mabasi, shule na hospitali kwa wilaya ya Morogoro pekee,



"...kwa leo nimetembelea miradi ya bilioni 39 na nusu kwa wilaya moja ya Morogoro ni fedha nyingi tunapaswa kumshukuru sana Mhe. Rais..." amesema Prof. Shemdoe.
Aidha huku ametoa agizo kwa Wakurugenzi Watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa hapa nchini kuhakikisha kuwa fedha zinazotolewa na Serikali zinapaswa kusimamiwa kwa uadilifu, uwazi na weledi ili kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa wakati, kwa viwango vilivyokusudiwa na kuleta tija kwa wananchi waliokusudiwa kunufaika.
Naye, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amemuhakikishia Waziri huyo wa TAMISEMI kuwa Mkoa umejipanga kuhakikisha wanaimarisha mifumo ya usimamizi na ufuatiliaji wa miradi ili kuondoa mianya ya ubadhirifu na uzembe.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Morogoro Mhe. Sebastian Waryuba kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi Watendaji wameahidi kuyafanyia kazi maelekezo yaliyotolewa, wakiahidi kusimamia ipasavyo fedha za miradi.



Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero
Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO
Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348
Mobile: +255 23 293 4348
Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz
Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.