• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YAKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO SEKTA ZA AFYA, ELIMU

Posted on: January 22nd, 2026

Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Januari 22, 2026 wamefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika sekta za afya na elimu, ikiwa ni sehemu ya jukumu lake la kuhakikisha fedha za serikali zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na miradi inakamilika kwa ubora unaotakiwa.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa Halmashauri ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Koila Korman Majuka amesema ukaguzi huo unalenga kutathmini hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa miradi hiyo, changamoto zilizopo pamoja na kutoa maelekezo ya kuboresha utekelezaji ili wananchi wanufaike na huduma bora za afya na elimu.

Katika sekta ya afya, kamati imekagua mradi wa ukamilishaji wa Zahanati ya Kijiji cha Vitonga mbapo Serikali kuu imetoa kiasi cha shilingi milioni 63,755,910. Zahanati hiyo inatarajiwa kuwa mkombozi kwa wananchi wapatao 2112 ambao wamekuwa wakilazimika kutembea umbali wa kilometa 6 kufuata huduma ya Afya katika kituo cha Afya cha Mlali.

Kwa upande wa sekta ya elimu, kamati imetembelea mradi wa ujenzi shule mpya ya Sekondari ya Kata ya Mkindo shilingi milioni 528, ujenzi wa shule ya msingi WamiDakawa shilingi milioni 291, ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa pamoja na matundu ya vyoo milioni 66 katika shule ya msingi Mkuyuni na ukamilishaji wa vyumba viwili vya madarasa kupitia mapato ya ndani milioni 25 shule hiyo ya msingi Mkuyuni.

Aidha, Wajumbe wa Kamati hiyo wametembelea eneo la ujenzi wa Sekondari ya Kata ya Homboza kwa nguvu za wananchi huku Kamati hiyo ikitoa wito kwa wananchi kujitoa kuchangia kuendeleza ujenzi huo na kuahidi kuwa shule hiyo itajengwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MIPANGO, BAJETI ZA HALMASHAURI ZIENDANE NA DIRA YA MAENDELEO YA TAIFA 2050 - RC MALIMA

    January 27, 2026
  • DC MVOMERO ALIPONGEZA SHIRIKA LA SAWA KUJENGA MADARASA YA SHULE SHIKIZI, AAGIZA MCHAKATO WA USAJILI UANZE MARA MOJA

    January 23, 2026
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YAKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO SEKTA ZA AFYA, ELIMU

    January 22, 2026
  • WAZAZI/WALEZI WAELIMISHWE JUU YA UMUHIM WA CHAKULA SHULENI ILI WAHAMASIKE KUCHANGIA

    January 19, 2026
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.