• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WAZAZI/WALEZI WAELIMISHWE JUU YA UMUHIM WA CHAKULA SHULENI ILI WAHAMASIKE KUCHANGIA

Posted on: January 19th, 2026

Watendaji wa Kata katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero wametakiwa kuwaelimisha Wazazi na walezi kuhusu umuhimu wa uwepo wa chakula shuleni ili waweze kushiriki kikamilifu katika kuchangia mpango huo unaolenga kuboresha mazingira ya ujifunzaji kwa wanafunzi. Elimu hiyo itasaidia kuongeza uelewa juu ya mchango wa chakula katika kuimarisha mahudhurio ya wanafunzi, kuongeza umakini darasani na kuboresha ufaulu wa masomo.

Wito huo umetolewa Januari 19, 2026 na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya hiyo Mwl. Bruno Sangwa wakati wa kikao cha kamati ya lishe Wilaya kilichofanyika katika Ofisi ya Mganga Mkuu wa Wilaya.

Mwl. Sangwa amesisitiza kuwa chakula shuleni ni nyenzo muhimu ya kuwafanya wanafunzi kubaki shuleni muda wote wa masomo bila usumbufu wa njaa, hali inayochangia kupunguza utoro na kuongeza nidhamu. Aidha, ameeleza kuwa pale wazazi na walezi wanapopata elimu sahihi, huwa tayari kuchangia kwa hiari kupitia michango ya chakula au fedha kulingana na makubaliano ya jamii husika.

Aidha, ameongeza kuwa ushirikiano kati ya Watendaji hao, kamati za shule na wazazi ni nguzo muhimu ya kufanikisha mpango wa chakula shuleni. Kupitia uelewa huo jamii itaweza kuelewa wajibu wake katika kuhakikisha wanafunzi wanapata lishe bora inayowawezesha kusoma kwa afya na ari.

Kwa upande wake Afisa lishe Hospitali ya Wilaya ameeleza kuwa Halmashauri ilipanga kutumia kiasi cha shilingi milioni 59,843,017 kwa kipindi cha mwezi Julai – Disemba 2025 ambapo kila mtoto alitengewa shilingi 1925, Halmashauri ilitumia shilingi milioni 61,465,904 sawa na asilimia 102 huku akibainisha kuwa kila mtoto amepata kiasi cha shilingi 1977.

Nao baadhi ya Watendaji wa Kata akiwemo Mtendaji wa kata ya Mzumbe Amasha Mwamba ameishukuru Halmashauri kwa kuanda kikao hicho huku akiahidi kuwa wataendelea kufanya kazi kwa weledi ili kuhakikisha kuwa Wilaya ya Mvomero inakuwa kinara katika suala la lishe.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MIPANGO, BAJETI ZA HALMASHAURI ZIENDANE NA DIRA YA MAENDELEO YA TAIFA 2050 - RC MALIMA

    January 27, 2026
  • DC MVOMERO ALIPONGEZA SHIRIKA LA SAWA KUJENGA MADARASA YA SHULE SHIKIZI, AAGIZA MCHAKATO WA USAJILI UANZE MARA MOJA

    January 23, 2026
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YAKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO SEKTA ZA AFYA, ELIMU

    January 22, 2026
  • WAZAZI/WALEZI WAELIMISHWE JUU YA UMUHIM WA CHAKULA SHULENI ILI WAHAMASIKE KUCHANGIA

    January 19, 2026
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.