• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WAZIRI KIJAJI AWAHAKIKISHIA WAFUGAJI UPATIKANAJI WA MBEGU ZA MALISHO KWA AJILI YA MASHAMBA 1200 YA TUTUNZANE

Posted on: January 4th, 2025

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (MB) amemuhakikishia Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli upatikanaji wa mbegu bora za malisho kwa ajili ya mashamba 1,200 ya Wafugaji ambao wamekubali kujiunga kwenye Kampeni ya Tutunzane Mvomero.

Mhe. Kijaji ameyasema hayo Januari 4, 2024 wakati akizungumza na viongozi wa Mkoa na Wilaya ya Mvomero pamoja na baadhi ya watendaji wa Wizara hiyo mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mvomero kwa ajili ya ziara ya kikazi Wilayani humo.

Waziri huyo amesema changamoto inayowakabili wafugaji wengi ni suala la malisho ya uhakika na maji hususan wakati wa kiangazi, hivyo amesema Wizara itahakikisha mbegu hizo zinapatikana ili mashamba hayo 1200 ya wafugaji yapandwe na kwamba yatasaidia kupunguza migogoro ya wakulima na wafugaji.

“...narejea Naibu Katibu hili la mbegu tulale, tuamke lazima mbegu zipatikane za malisho...sisi sasa ndio muda wetu wa kutokulala na kutokuota mpaka tutakapo hakikisha wafugaji wote, mashamba yote 1200 yamepata mbegu..." amesema Dkt. Kijaji.

Aidha, Waziri Kijaji amesema zoezi hilo la ugawaji wa mbegu ni kuungamkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye aliizindua kampeni hiyo Agosti 3, 2024 hivyo watahakikisha hawamuangushi.

Sambamba na hilo amewataka wafugaji kufuga kisasa ili mifugo yao iwe na viwango vinavyohitajika katika masoko ya kimataifa huku akibainisha kuwa Mkoa wa Morogoro utakuwa kanda maalum ya mifugo na kwamba mapinduzi ya Sekta hiyo yataanzia Mkoani Morogoro.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amebainisha mipango ya Mkoa huo kwenye sekta ya mifugo ikiwemo kuufanya mnada wa Mkongeni kuwa Soko la kimataifa la mifugo huku akisema kuwa ili kufikia huko wafugaji wanatakiwa kuwa na mifugo yenye viwango.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amesema upatikanaji wa mbegu za malisho pamoja na gharama za uchimbaji wa visima ni changamoto mojawapo katika utekelezaji wa kampeni hiyo. Aidha, amesema wakati kampeni hiyo inaanza kulikuwa na mashamba 379 ambayo yalipatiwa hati lakini kutokana na kukosekana kwa mbegu yalipandwa mashamba 42 pekee, hadi sasa wafugaji 1202 wamehamasika kuandaa mashamba.

                                                                                           

 MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.