• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WATUMISHI HALMASHAURI YA WILAYA YA MVOMERO WATAKIWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO IPASAVYO

Posted on: February 20th, 2025

Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi, uwajibikaji, na uadilifu ili kumsaidia Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri pamoja na  kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Agizo hilo limetolewa Februari 20, 2025 na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mhe. Yusuph Makunja wakati akifungua mkutano wa kawaida wa baraza la Madiwani lililolenga kujadili taarifa za Robo ya Pili kwa kipindi cha Oktoba - Desemba 2024, mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Makunja amesisitiza umuhimu wa kila mtumishi kujituma na kufanya kazi kwa bidii katika idara yake ili kuhakikisha maendeleo ya Wilaya na ya wananchi yanapiga hatua.

"...naomba ndugu zangu wataalam na watendaji wa Halmashauri fanyeni kazi ile ambayo inayotakiwa katika shughuli zetu za kawaida na maelekezo ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania..." amesisitiza Mhe. Makunja.

Aidha, amewataka Watumishi wa Halmashauri hiyo kutoa ushirikiano kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bi. Loema Peter ambaye ameaminiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwatumikia wananchi wa Mvomero.

Sambamba na hilo, Mwenyekiti huyo wa Halmashauri amempongeza Mkurugenzi kwa maono mazuri ambayo anaamini yataivusha Halmashauri hiyo kwenda kwenye hatua nyingine ya maendeleo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amewaomba Waheshimiwa Madiwani kumpokea Mkurugenzi huyo mpya na kumpa ushirikiano wa kutosha ili kuhakikisha kuwa malengo ya Halmashauri yanatimia.

Mhe. Nguli amewasisitiza Watumishi na watendaji kumsaidia na kupokea mabadiliko, mipango na mikakati ya kuitoa Halmashauri hiyo mahali ilipo sasa na kuipeleka kwenye Mvomero ya mafanikio.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • JAMII YATAKIWA KUSHIKAMANA KUPINGA MILA ZINAZOATHIRI HAKI ZA MTOTO

    June 16, 2025
  • MVOMERO YAPONGEZWA KUONESHA JUHUDI UFUATILIAJI MADENI YA MIKOPO YA VIKUNDI

    June 12, 2025
  • WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MVOMERO WAPEWA SIKU 7 KULIPA MADENI YA MSD

    June 05, 2025
  • UWEPO KAZINI, KUFIKA KWA WAKATI NA KUFANYA KAZI KWA BIDII NI MSINGI WA HUDUMA BORA

    June 05, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.