• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WANAOCHUKUA PIKIPIKI ZA MKATABA WASHAURIWA KUSHIRIKISHA VIONGOZI WA SERIKALI ZA VIJIJI KUEPUSHWA UKIUKWAJI WA MIKATABA NA MASHARTI MAGUMU

Posted on: December 8th, 2025

Wananchi wanaochukua pikipiki kwa mikataba ya makubaliano na wamiliki wake wameshauriwa kuhakikisha wanashirikisha viongozi wa serikali za vijiji wakiwemo watendaji wa Vijiji ili kuzuia migogoro isiyo ya lazima pamoja na ukiukwaji wa masharti ya mkataba.


Ushauri huo umetolewa Disemba 08, 2025 na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Maulid Dotto wakati akizungumza na Maafisa Wasaririshaji (Boda boda) wa Kata za Mzumbe na Mlali.


Mhe. Maulid Dotto ameeleza kuwa kumekuwa na ongezeko la malalamiko kati ya wamiliki wa pikipiki na waendeshaji wanaochukua vyombo hivyo kwa mkataba bila kuwepo kwa usimamizi wa serikali za vijiji.


Aidha, amesema kuwa ushirikishwaji wa uongozi wa kijiji utasaidia kuweka kumbukumbu sahihi za makubaliano, kuongeza uwajibikaji, na kuhakikisha pande zote mbili zinazingatia taratibu zilizowekwa. Hata hivyo, hatua hiyo itarahisisha utatuzi wa migogoro iwapo kutatokea uvunjifu wa masharti ya mkataba.


Kwa upande wake Askari Kata wa kata ya Mazumbe Afande Selenda amewashauri Maafisa Wasafirishaji hao kutunza kumbukumbu za malipo wanayofanya kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri ili kuepusha migogoro ya inayoweza kutokea.


Nao baadhi ya Maafisa wasafirishaji hao wamesema kuna baadhi ya wamiliki wa vyombo vya usafiri wamekuwa sio waaminifu na wengine wamekuwa wakiweka masharti magumu, huku akiongeza kuwa wengi wao wanaingia mikataba hiyo kwa sababu wamekosa shughuli nyingine za kufanya ili kujiingizia kipato.


MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KUONEKANA KWA KAKAKUONA ISHARA YA NEEMA KWA WANANCHI MVOMERO, DC AWASHUKURU KUTOA TAARIFA KWA WAKATI

    December 10, 2025
  • WANAOCHUKUA PIKIPIKI ZA MKATABA WASHAURIWA KUSHIRIKISHA VIONGOZI WA SERIKALI ZA VIJIJI KUEPUSHWA UKIUKWAJI WA MIKATABA NA MASHARTI MAGUMU

    December 08, 2025
  • MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA MVOMERO WATAKIWA KUWA NA NYENZO NNE MUHIMU ZA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    December 05, 2025
  • DAS MVOMERO AWATA WAHESHIMIWA MADIWANI KUTUMIA MUDA WAO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI KATIKA MAENEO YAO

    December 05, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.