• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

Posted on: April 26th, 2025

Katika kuadhimisha miaka 61 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, wananchi wametakiwa kuendelea kudumisha amani na utulivu pamoja na kuwapuuza watu wanaochochea uvunjifu wa amani iliyopo.

Wito huo umetolewa leo Aprili 26, 2025 na Katibu Tawala wa Wilaya ya Mvomero Ndg. Said Nguya wakati wa hafla ya Maadhimisho ya Miaka 61 ya Muungano ambapo kiwilaya maadhimisho hayo yamefanyika katika shule ya Sekondari Sokoine Memorial.

"...tuwapuuze wale ambao wanaleta chokochoko kwa maslahi yao binafsi, nchi yetu imeendelea kuwa kisiwa cha amani tangu enzi za Waasisi wetu Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Hayati Abeid Amani Karume, tuitunze tunu hiyo..." amesema Ndg. Nguya.

Aidha, amewataka vijana kuwa makini na watu ambao wamekuwa wakiwashawishi vijana kufanya vulugu kwa maslahi yao ya kisiasa huku akiwataka kuripoti taarifa za viashiria vya uvunjifu wa amani.

Kwa upande wake Afisa Kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Bw. Mohamed Longoi akimuwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo amewashukuru Viongozi, Watumishi, Wanafunzi pamoja na wananchi waliojitokeza kuadhimisha sherehe za Muungano kwa kushiriki kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo usafi na upandaji miti.

Sambamba na hilo, amewahimiza wananchi kujitokeza kushiriki uchaguzi Mkuu ambao unatarajiwa kufanyika mwaka huu 2025.

Naye Kaimu Afisa elimu Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mwl. Shangweli ameushukuru uongozi wa Wilaya na Halmashauri kwa kuchagua shule ya Sekondari ya Sokoine Memorial kuadhimisha sherehe za Muungano ngazi ya Wilaya. Aidha, amewataka walimu na wanafunzi kutunza miti ambayo imepandwa shuleni hapo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa mwaka huu 2025 zimepambwa na kaulimbiu isemayo "Miaka 61 ya Jamhuri ya Muungano: Muungano wetu ni dhamana, Heshima na Tunu ya Taifa: Shiriki uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025..."

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.