• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WANANCHI WATAKIWA KUUNGA MKONO JITIHADA ZA SERIKALI KUONGEZA UZALISHAJI SEKTA ZA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI

Posted on: August 2nd, 2024

Wito umetolewa kwa wananchi kuendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali kwa kushirikiana wadau ili kuleta matokeo chanya kwa kuongeza uzalishaji, ubora na usindikaji wa mazao ya mifugo, kilimo na uvuvi.

Wito huo umetolewa Agosti 2, 2024 na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Balozi Dkt. Batilda Buriani wakati wa uzinduzi wa Maonesho ya Nane nane Kanda ya Mashariki 2024 uliofanyika katika viwanja vya maonesho vya Mwl. J. K. Nyerere vilivyopo katika Manispaa ya Morogoro.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema wananchi wakiongeza uzalishaji itasaidia nchi kuendelea kuwa na usalama wa chakula na lishe bora, kuongeza upatikanaji wa malighafi za viwandani, kuongeza mazao nje ya nchi, kuongeza ajira kwa wananchi pamoja na kuchochea mchango wa Sekta za kilimo, mifugo na uvuvi kwenye  pato la Taifa.

"...wito wangu kwenu ni tuendelee kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali kwa kushirikiana na wadau ili kuleta matokeo chanya..." amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha, amebainisha kuwa Sekta hizo zina  mchango katika upatikanaji wa ajira kwa wananchi ambapo zaidi ya asilimia 65 ya watanzania wanajishughulisha na sekta hizo, vile vile zinachangia asilimia 28 ya pato la Taifa pia zinachangia asilimia 24 ya mauzo ya bidhaa zinazotokana na mazao ya sekta hizo nje ya nchi. Lakini pia zina imarisha usalama wa chakula na lishe bora.

Sambamba na hilo, Dkt. Buriani ameeleza mikakati ya Seikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutatua changamoto zilizopo kwenye Sekta hizo ikiwemo uhamasishaji wa matumizi ya teknolojia zinazolenga kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Rufiji Meja Edward Kiwele akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani amesema maonesho ya Nane nane kanda ya mashariki 2024 lengo lake ni kutoa fursa kwa wakulima, wafugaji na wavuvi kujifunza mbinu mbalimbali za teknolojia mpya zinazoongeza tija na kuleta mabadiliko chanya katika sekta hizo muhimu kwa usalama wa chakula na uchumi wa Taifa.

Ameongeza kuwa hadi kufikia Julai 30, 2024 zaidi ya washiriki 596 wamethibisha kushiriki katika maonesho hayo kwa mwaka huu ikilinganishwa na washiriki 589 mwaka 2024 huku akisema kuwa watu zaidi ya 80000 wanatarajiwa kutembelea maonesho hayo kwa lengo la kujifunza teknolojia mbalimbali za kilimo, ufugaji na uvuvi.

Maonesho ya Nane nane 2024 kitaifa yanafanyika Mkoani Dodoma huku yakiwa na kaulimbiu isemayo "Chagua Viongozi bora wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo endelevu ya Kilimo, Mifugo na  Uvuvi.

MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.