• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA KUPATA MATIBABU YA KIBINGWA HOSPITALI YA WILAYA

Posted on: October 16th, 2024

Wananchi wa Wilaya ya Mvomero wametakiwa kujitokeza kwa wingi kupata huduma za matibabu ya kibingwa zinazotolewa katika Hospitali ya Wilaya hiyo, huduma hizo ni sehemu ya jitihada za serikali za kuboresha afya za wananchi na kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa kila mtu.

Wito huo umetolea mapema hii leo Oktoba 16, 2024 na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli wakati wa uzinduzi wa Kambi Maalum ya Madaktari Bingwa wa Mama Samia awamu ya pili inayoendelea katika Hospitali ya Wilaya pamoja na kukabidhi gari kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji wa huduma za afya.

Mhe. Nguli amesema kuwa matibabu hayo yatahusisha wataalamu bingwa kutoka sekta mbalimbali za afya, wakiwemo madaktari bingwa wa magonjwa ya ndani, upasuaji, magonjwa ya Wanawake na uzazi, usingizi na magonjwa ya watoto pamoja na magonjwa ya kinywa na meno huku akisisitiza kuwa huduma hizo zitakuwa za gharama nafuu na zingine zitatolewa bure ili kuhakikisha wananchi wote wanapata fursa ya matibabu.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya amewataka wananchi kutumia nafasi hii muhimu kujitokeza kwa wingi na kuhamasishana kwani Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imewasogezea huduma karibu na kuwapunguzia adha ya kusafiri umbali mrefu na gharama kubwa kufuata huduma za kibingwa katika hospitali kubwa.

Sambamba na hayo, Mhe. Nguli amewataka wajumbe wa timu ya usimamizi wa huduma za Afya katika hospitali hiyo (CHMT) kutumia gari walilokabidhiwa kama ilivyokusudiwa na hatimaye kuleta matokeo chanya katika huduma hizo za Afya.

Awali wakati akimkaribisha Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mwl. Linno Mwageni amesema uwepo wa Madaktari Bingwa wa Mama Samia imekuwa ni faraja kwa wananchi wa Wilaya hiyo kwani imerahisisha upatikanaji wa huduma za kibingwa karibu na wananchi hao.

Aidha, Mwl. Linno amemshukuru Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha huduma za afya katika Wilaya hiyo hususan katika hospitali ya Wilaya na kwamba Halmashauri itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za afya katika Wilaya hiyo.

Naye, Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Dkt. Alex Mzava amesema wamepokea Madaktari Bingwa saba huku akibainisha kuwa mwitikio wa wananchi ni mkubwa kwani tangu kuanza kwa kambi hiyo wananchi wanaendelea kujitokeza kwa wingi.

Kwa upande wake Dkt. Beatus ambaye ni  Daktari bingwa wa magonjwa ya kinywa na meno, kwa niaba ya Madaktari hao amesema lengo la uwepo wao ni kusogeza huduma za kibingwa karibu na wananchi wa Wilaya ya Mvomero pamoja na kuwajengea uwezo Madaktari waliyopo katika hospitali hiyo ili kuendeleza huduma hizo pindi wao watakapo ondoka.

Madaktari Bingwa wa Mama Samia wameanza kutoa matibabu ya kibingwa katika hospitali ya Wilaya kuanzia Oktoba 14 na wataendelea hadi Oktoba 20, 2024.

MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.