• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WANANCHI WAHIMIZWA KUCHANGAMKIA KILIMO CHA MAZAO YA VIUNGO

Posted on: May 9th, 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa ameendelea kuwahimiza wananchi Wilayani Mvomero kuchangamkia kilimo cha mazao ya viungo kwa kuwa yanafaida katika kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja, Wilaya na Mkoa kwa ujumla.

Dkt. Mussa ametoa wito huo Mei 9, 2024 wakati wa zoezi la ugawaji wa miche 500 ya Karafuu kwa wananchi wa Vijiji vya Mnyanza na Tangeni vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero ikiwa ni muendelezo wa kampeni ya kuhamasisha wananchi Mkoani Morogoro kulima mazao ya viungo kama vile Karafuu, Vanila, kokoa, Iriki na Mdalasini.

Katibu Tawala huyo amesema lengo la Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan na Chama cha Mapinduzi – CCM ni kuboresha maisha ya watanzania kupitia nyanja mbalimbali kama vile kilimo, hivyo amewataka wananchi wa Vijiji vya Tangeni, Mnyanza na maeneo mengine  kuchangamkia fursa zinazotolewa na Serikali ambazo zinalenga kuboresha maisha yao.

“...maneno yetu yachukueni na ninyi fanyeni kwa sababu tunachokifanya ni kuwaachia rasilimali ambayo itawasaidia ninyi wenyewe na vizazi vyenu...” amesema Dkt. Mussa.

Aidha, Dkt. Mussa amebainisha uwepo wa masoko ya uhakika wa mazao hayo ya viungo.

Katika hatua nyingine, Katibu Tawala huyo ameendelea kuwasisitiza wakulima kuwakwepa madalali ambao wamekuwa mwiba kwa wakulima kushindwa kufikia malengo ya kukuza uchumi.

Naye Afisa Kilimo kutoka Halmashauri ya Wilaya Mvomero Bi. Consolata Tarimo amesema Wilaya ya Mvomero ni miongoni mwa Wilaya zinazolima zao la Karafuu ambapo hadi sasa Wilaya imepokea miche 1000 ya zao hilo ambayo imegawanywa katika vijiji vya Mnyanza, Tangeni na vijiji vingine vinavyozalisha karafuu.

Ameongeza kuwa Halmashauri imeanzisha kitalu cha miche ya karafuu 12000 katika Kata ya Mhonda huku akibainisha kuwa wananchi wamelipokea kwa mikono miwili zao hilo la Kimkakati.

Kwa upande wao wananchi waliopokea miche hiyo akiwemo Bw. Mustafa Salum ameishukuru Serikali kwa kuwapatia fursa hiyo ambayo itainua uchumi wao. Pamoja na kuipongeza Serikali Bw. Mustafa amemshukuru Katibu Tawala huyo kwa kuhakikisha kuwa wananchi Mkoani Morogoro wananufaika na kilimo cha mazao ya viungo.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.