• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WANANCHI WAASWA KUTOGOMEA MIRADI YENYE TIJA KWENYE UCHUMI

Posted on: July 16th, 2025

Wananchi wametakiwa kuepuka tabia ya kugomea au kupinga utekelezaji wa miradi yenye manufaa kwao na taifa kwa ujumla, bali washirikiane kikamilifu na Serikali pamoja na wadau ili kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa na kuleta matokeo chanya katika ustawi wa uchumi wa jamii.

Wito huo umetolewa Julai 16, 2025 na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Me. Maulid Dotto wakati akizungumza na Viongozi pamoja na wananchi wa kijiji cha Gonja.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema kuwa miradi ya uwekezaji ikiwemo mradi wa uboreshaji wa msitu wa Kijiji cha Gonja unaotekelezwa na Shirika la PAMS Foundation unalenga kutoa fursa mbalimbali ikiwemo za kiuchumi hivyo ametoa wito kwa viongozi na wananchi wa kijiji hicho kuacha tabia ya kuzuia miradi kama hiyo ambayo itawanufaisha wananchi wengi.


"...mradi huu wa PAMS Foundation unafursa nyingi za kiuchumi na kijamii tuache kuzuia zuia vitu ambavyo vinakwenda kusaidia watu..." amesema Mhe. Maulid Dotto.


Aidha, ameongeza kuwa zipo sheria mbalimbali za utunzaji wa mazingira, ardhi na misitu ambapo kila kiongozi, mwananchi anawajibu wa kuzifuata na kuzitekeleza.


Sambamba na hilo, Mkuu huyo wa Wilaya amewataka Viongozi wa Serikali ya kijiji cha Gonja na wananchi wa kijiji hicho kuupokea kwa mikono miwili mradi wa uboreshaji wa msitu wa Kijiji hicho ili waweze kukuza uchumi wao.


Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Ndg. Paulo Faty amesema kuwa wananchi ndiyo wenye maamuzi katika matumizi ya rasilimali za vijiji kupitia mkutano Mkuu wa Kijiji huku akibainisha kuwa Serikali ya kijiji haina mamlaka ya kufanya maamuzi bila mkutano mkuu wa wananchi.


Naye Afisa Misitu kutoka Halmashauri hiyo amesema kuwa Mkuu wa Wilaya aliunda timu ya kupitia upya mpango wa matumizi bora ya ardhi katika kijiji hicho na kutoa mapendekezo mbalimbali ikiwemo uwekaji wa alama za kudumu katika mipaka ya msitu huo ili kuzuia uvamizi unaofanywa na wananchi.


Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MZUMBE UNIVERSITY YAUNGA MKONO KAMPENI YA MAMA SAMIA LEGAL AID, YAKABIDHI VITABU 400 VYA SHERIA

    July 21, 2025
  • PAMS FOUNDATION YAPONGEZWA KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    July 19, 2025
  • RAS MOROGORO ARIDHISHWA NA MRADI WA UBORESHAJI MISITU, AMUAGIZA DED MVOMERO KUSHUGHULIKIA SUALA LA HATI

    July 17, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUTOGOMEA MIRADI YENYE TIJA KWENYE UCHUMI

    July 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.