• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WANANCHI WAASWA KUCHANGIA HUDUMA ZA MAJI KATIKA MAENEO YAO.

Posted on: May 20th, 2024

Wananchi Wilayani Mvomero wameaswa kuchangia huduma ya maji inayopatikana katika maeneo yao na kwamba fedha hizo wanazochangia zinasaidia katika kuboresha upatikanaji wa huduma hiyo kwenye maeneo husika.

Wito huo umetolewa Mei 20, 2024 na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mhe. Yusuph Makunja wakati akifungua Warsha ya mradi wa kuboresha huduma ya Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini kwa ubia kati ya Serikali na Sekta binafsi. Warsha hiyo imefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.

Mhe. Makunja amesema kuwa Serikali imetumia gharama katika kuwapelekea wananchi wake huduma ya maji safi na salama hapa nchini ili waondokane na matumizi ya maji yasiyo salama kwa afya zao lakini baadhi ya wananchi wanaharibu miundombinu hiyo na kugoma kulipia huduma hiyo muhimu huku akisema kuwa kitendo hicho ni kurudisha nyuma juhudi za Serikali katika kuwaletea wananchi wake maendeleo.

Aidha, Mweyekiti huyo amewataka wananchi kuipa kipaumbele huduma ya maji kutokana na umuhimu wake katika maisha ya mwanadamu.

“...tusimame kama viongozi wa Serikali tuwape mafunzo wananchi wetu, tuwape maelekezo ikiwezekana tuweze kulipia maji kabla ya matumizi ili tuondokane na changamoto ya upatikanaji wa maji kwenye maeneo yetu...” amesema Mhe. Makunja.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo wa Halmashauri ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Sekta binafsi katika kutatua changamoto ya upatikanaji wa Maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero na kuanzisha mradi wa kuboresha huduma ya maji na usafi wa mazingira Wilayani humo.

Naye, Mratibu wa zoezi la ushirikishwaji jamii katika mpango wa Serikali wa ushirikishaji Sekta binafsi katika miradi ya maji Vijijini Bw. Emmanuel Burton amesema zoezi hilo la usshirikishwaji jamii linafanyika katika mikoa mitano ya Kagera, Morogoro, Lindi, Dodoma na Manyara ambapo Wilay 15 zimechaguliwa kwa ajili ya kuanza kwa mradi huo.

Aidha, Bw. Burton amebainisha changamoto ambazo zimepelekea kushindwa kufikia lengo la asilimia 85 katika upatikanaji wa huduma ya maji vijijini ambapo kwa sasa wamefikia asilimia 77, changamoto hizo ni pamoja na uhaba wa rasilimali fedha, upungufu wa rasilimali watu. Pamoja na hayo amesema wananchi kushindwa kuchangia huduma ya maji kunapelekea ugumu katika uboreshaji wa miundombinu ikiwemo mabomba na vichotea maji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya watumia maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Bi. Ezdonia Batholomeo amewashukuru wawezeshaji wa warsha hiyo ambapo amesema itasaidia kuboresha vyombo vya watumia maji vilivyopo Wilayani humo.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAPONGEZWA KUONESHA JUHUDI UFUATILIAJI MADENI YA MIKOPO YA VIKUNDI

    June 12, 2025
  • WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MVOMERO WAPEWA SIKU 7 KULIPA MADENI YA MSD

    June 05, 2025
  • UWEPO KAZINI, KUFIKA KWA WAKATI NA KUFANYA KAZI KWA BIDII NI MSINGI WA HUDUMA BORA

    June 05, 2025
  • MVOMERO KUTUMIA SHERIA NDOGO KUWABANA WAZAZI WASIOCHANGIA CHAKULA SHULENI

    June 02, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.