• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WANANCHI MVOMERO WAMSHUKURU RAIS SAMIA

Posted on: January 5th, 2023

Wananchi wa vijiji vya Lubungo na Mingo ambavyo vipo Kata ya Lubungo Tarafa ya Mlali  Wilayani Mvomero Mkoa wa Morogoro vyenye jumla ya wananchi wapatao 2016 wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia mradi wa maji na hivyo kuondokana na adha ya maji.

Kabla ya mradi huo  walilazimika kutembea kilomita zaidi ya 10 kufuata maji kwenye mito na mabwawa huku wakihatarisha maisha yao kwani eneo hilo linapakana na Mbuga ya Mikumi eneo ambalo lina wingi wa tembo.

Hayo yameelezwa na Diwani wa Kata ya Lubungo Hamidu Zuberi kwenye ufunguzi wa Mradi wa maji wa Lubungo ulioghalimu zaidi milioni 400 fedha zilizotolewa na Mfuko wa Maji (NWF) na kutekelezwa na RUWASA.

Alisema utekelezwaji wa Mradi huo umeenda kumshusha Mama ndoo kichwani kwa sasa wananchi hawachangii tena maji na Tembo kama hapo awali na kwamba wameshapoteza wapendwa wao 4 na wengine kupata ulemavu wakati wakienda kwenye mito na mabwawa.

“Nimshukuru sana Mama yetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa fedha hizi za mradi wa maji kata ya Lubungo kiukweli Mama ametuheshimisha mimi pamoja na Mbunge wangu Mhe. Zeeland sasa tunapita kifua mbele.” alisema Mheshimiwa Diwani.

Akizungumza kwenye mkutano wa adhara na wananchi wa Kata ya Lubungo Waziri wa Maji Jumaa Aweso aliwahakikishia wananchi wa Wilaya ya Mvomero na Mkoa wa Morogoro kwa ujumla kuwa Serikali ya awamu ya sita kupitia Wizara ya maji itahakikisha kila mwananchi anapata maji safi na salama.

Aidha aliwataka wananchi walio karibu na mradi wa maji kuulinda na kuutunza ili waendelee kupata huduma ya maji safi na salama kila wakati kwani Serikali inatumia fedha nyingi katika kutekeleza miradi hiyo ili wananchi waweze kupata maji.

Kwa upande wake, Meneja wa RUWASA Wilayani Mvomero, Mhandisi Sospeter Lutonja akitoa taarifa juu ya mradi huo alisema kuwa mradi huo umetekelezwa na Kampuni ya CHAKWELE CO. LTD ulianza 04.10.2018 na kukamilika rasmi 22.11.2021 unahudumia wananchi zaidi ya 2000. Mradi huo umegahrimu kiasi cha shilingi za Kitanzania 417,078,804.52 ambapo mkandarasi tayari ameshalipwa kiasi cha shilingi 406,460,795.18.

Utekelezaji wa mradi huo ulijumuisha ujenzi wa tanki la maji ujazo wa 90,000, mnara wa mita 6, ununuzi na ulazaji wa mabomba umbali wa mita 4020, ujenzi wa vituo 16 vya kuchotea maji pamoja na ununuzi na ufungaji wa mitambo ya nishati ya jua 9KW.

Hisani : RUWASA Tanzania / Farida Mangube

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • UWT MVOMERO WAKABIDHI BIMA YA AFYA KWA MTOTO OMARY KIYONDO

    May 30, 2025
  • WITO UMETOLEWA KWA WADAU, SERIKALI KUONGEZA JUHUDI KATIKA UTOAJI ELIMU YA HEDHI SALAMA VIJIJINI

    May 28, 2025
  • WAHE. MADIWANI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA WATEMBELEA MVOMERO KUJIFUNZA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI UNAVYOWAKOMBOA WAKULIMA WA KAKAO

    May 24, 2025
  • MVOMERO KUUZA UFUTA KUPITIA STAKABADHI GHALANI KUANZIA MEI 20, 2025

    May 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.