• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WANANCHI KITONGOJI CHA MAJICHUMVI WAISHUKURU ROTARY KWA KUSAIDIA UPATIKANAJI WA MAJI

Posted on: September 27th, 2024

Wananchi wa Kitongoji cha Majichumvi wametoa shukrani zao kwa Shirika la Rotary kwa msaada mkubwa wa kuimarisha upatikanaji wa maji safi na salama katika kitongoji hicho ambapo shirika hilo limechimba kisima ambacho kinatoa lita 20000 kwa masaa mawili mradi ambao umegharimu dola za Marekani 5200.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya mradi huo wa maji leo Septemba 27, 2024 katika Shule ya Msingi Majichumvi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Dakawa Mhe. Yusuf Makunja amesema mradi huo umeleta faraja kubwa kwa wakazi wa kitongoji hicho ambao kwa muda mrefu walikuwa wakikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama.

Aidha, Mhe. Makunja amelishukuru shirika hilo kwa msaada huo huku akiliomba kuendelea kutoa msaada katika maeneo mengine yenye changamoto ya upatikanaji wa maji.

"...kwa hesabu za haraka haraka haya maji yamepatikana kwa milioni 13 na pointi za kitanzania, ela si ndogo sisi tunawashukuru sana..." amesema Mhe. Makunja.

Katika hatua nyingine, Mhe. Makunja akiwa kama Diwani wa Kata ya Dakawa  ameahidi kuchangia umaliziaji na ukarabati wa ofisi ya walimu katika shule ya Msingi Majichumvi.

Naye, Mwakilishi wa shirika la Rotary amesema Rotary ni shirika la Kijamii linajihusisha  na kusaidia maendeleo ya jamii pia kila mtu ana nafasi ya kujiunga ikiwa tu analengo la kuisaidia jamii kimaendeleo, shirika hilo linajumuisha watu wa kada mbalimbali ambapo huchangishana fedha ambazo zinapelekwa kwenye jamii yenye uhitaji.

Ameongeza kuwa mradi wa kisima katika kitongoji cha Majichumvi umegharimu kiasi cha dola 5200 za Marekani ambazo ni sawa shilingi milioni 13 za kitanzania. Hata hivyo, ameahidi kuwa Rotary itaendelea kutoa ushirikiano  ili kuleta maendeleo katika jamii.

Miongoni mwa wananchi waliotoa shukrani zao kwa shirika hilo ni pamoja na Bi. Immaculata Charles mkazi wa Kitongoji cha Majichumvi amesema changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama ilipelekea wao kutumia maji ya miferejini ambayo sio salama kwa afya zao.

Nao wanafunzi wa Shule ya Msingi Majichumvi akiwemo Subira Rafael ameshukuru kupata huduma hiyo ya maji ambayo itawasaidia kutumia muda mwingi kusoma.

Katika hafla hiyo ya kukabidhi mradi wa maji kwa wananchi Mhe. Diwani pia alikabidhi jezi seti moja pamoja na mpira mmoja kwa timu ya vijana ya kitongoji hicho.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.