• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WAKULIMA WASHAURIWA KUTUMIA MBEGU BORA ZENYE TIJA KUTOKA TARI

Posted on: July 25th, 2024

Wakulima wa zao la mpunga Wilayani Mvomero wameshauriwa kutumia mbegu bora na zenye zinatija ya uzalishaji ambazo zimefanyiwa utafiti na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo TARI ili kuongeza uzalishaji na kukuza vipato vyao.

Ushauri huo umetolewa Julai 22, 2024 na Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmasahuri ya Wilaya ya Mvomero Bw.  Mohamed Longoi kwenye siku ya Mkulima shambani iliyoandaliwa na TARI katika Kijiji cha Mbogo kilichopo Wilayani humo.

Bw. Longoi amebainisha kuwa kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi hivyo wakulima hawanabudi kubadilisha mfumo wa uzalishaji wa zao hilo ili kuendana na mahitaji ya soko.

"...usipande ilimrdadi mbegu, panda mbegu bora..." amesema Afisa Kilimo.

Aidha, amewataka wakulima kushirikiana na wataalam wa kilimo, Taasisi, Serikali, Mashirika ya Umma na wadau mbalimbali ambao wanamchango chanya katika kukuza sekta ya kilimo.

Sambamba na hilo, Afisa Kilimo huyo amesema baadhi ya wakulima wamekuwa na mwitikio chanya kwenye ufuatiliaji wa kilimo cha kisasa ambacho kina ongeza uzalishaji wa zao hilo.

Naye, Mtafiti wa Kilimo kutoka TARI kituo cha Dakawa Bi. Fabiola Langa amesema Taasisi ya TARI Dakawa imejikita katika kutafiti wa kugundua mbegu bora za mpunga na Teknolojia mbalimbali za kilimo ambazo zinaongeza tija kwa wakulima na wadau hususan kwenye zao la mpunga.

Bi. Fabiola ameongeza kuwa hadi sasa wamegundua mbegu bora za mpunga zaidi ya 20 ambazo tayari zimethibitishwa kwa kutumiwa na wakulima. Akitolea mfano wa mbegu ya 'SARO FIVE' ameeleza kuwa mbegu hiyo inapendwa na wakulima pamoja na wadau wa mpunga kutokana na kuongeza tija ya uzalishaji na kipatao kwa wakulima.

Nao wakulima wa zao la mpunga katika Skimu ya Umwagiliaji ya Mbogo kwa Mtonga akiwemo Bw. Ally Palainda ameishukuru TARI kwa kuwapatia mafunzo na mbegu bora ambazo zitawasaidia kuongeza uzalishaji. Pia ameiomba Serikali kuwwajengea miundombinu bora ya Umwagiliaji kutokana na skimu hiyo kuwa ya kienyeji ambapo wamekuwa wakipata changamoto hususan wakati wa mvua ambayo uharibu miundombinu yao.

Skimu ya Umwagiliaji ya Mbogo kwa Mtonga ina zaidi ya ekari 9500 huku ikiwa na wakulima ziadi ya 9000.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.