• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WAFUGAJI 702 WAHAMASIKA KAMPENI YA TUTUNZANE MVOMERO, WADAU WASIFU JUHUDI ZA DC NGULI.

Posted on: August 1st, 2024

Ni muda mfupi tangu kuanzishwa kwa kampeni ya Tutunzane Mvomero ambapo hadi sasa zaidi ya wafugaji 702 wamehamasika kujiunga na kampeni hiyo ambayo imelenga kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji pamoja na utunzaji wa mazingira.

Hayo yamebainishwa Agosti 1, 2024 na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli wakati wa kikao cha wadau wa Sekta za mifugo na kilimo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.

Mhe. Nguli amesema tangu kuanzishwa kwa kampeni hiyo imewezesha wafugaji hao 702 kupimiwa ardhi na kupata hati zao, aidha, ameongeza kuwa kuna mashamba 42 ambayo yamepandwa malisho huku akibainisha kuwa changamoto iliyopo ni upatikanaji wa mbegu kwa ajili ya wafugaji wengine wenye mashamba kupanda malisho yao.

Pia amesema ujio wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan unatarajiwa kuwa suluhu ya changamoto hiyo ya mbegu.

“...zaidi ya wafugaji 702 wamo kwenye kampeni ya tutunzane, sasa tuna idadi kubwa ya watu waliohamasika kwa muda mfupi...” amesema Mkuu wa Wilaya.

Sambamba na hilo, Mhe. Judith Nguli amebainisha kuwa Kampeni hiyo sasa itakuwa endelevu kwani umeandaliwa mpango wa miaka mitano yaani kuanzia mwaka huu 2024 hadi 2028 lengo ni kuhakikisha kuwa kampeni hiyo inawafikia wafugaji wengi ili kumaliza kabisa migogoro katika Wilaya hiyo. Pia ameishukuru Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa ushirikiano mzuri tangu kuanzishwa kwa kampeni hiyo.

Naye Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Daniel Mushi ameipongeza Wilaya ya Mvomero kwa kuwa mfano wa kuigwa katika kupambana na migogoro ya wakulima na wafugaji kwa kutumia mbinu za kisayansi. Aidha, ameeleza mikakati ya Serikali katika kukabiliana na wingi wa mifugo hapa nchini ikiwemo kuhimiza wafugaji kuvuna mifugo yao ili waweze kuihudumia kwa urahisi.

Kwa upande wake Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Shekhe Twaha Kilango amempongeza Mkuu wa Wilaya hiyo kwa ushirikiano anao utoa kwa viongozi wa dini pamoja na kamati za Maridhiano katika kushughulikia migogoro ya wakulima na wafugaji huku akisema kuwa Amani na utulivu uliopo Mvomero kwa sasa ni matokeo ya  ushirikiano uliopo.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.