• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WADAU WA MAENDELEO WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO KWA TIMU YA WATAALAM WA ARDHI.

Posted on: April 22nd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amewataka wadau wa maendeleo Wilayani humo kutoa ushirikiano kwa timu ya wataalam wa ardhi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa ajili ya kufanikisha mradi wa uboreshaji usalama wa milki za ardhi ardhi ambao unatarajia kufanyika Wilayani humo.

Mhe. Nguli ameyasema hayo Aprili 22, 2024 wakati akifungua Mkutano wa wadau kujadili utekelezaji wa mradi wa uboreshaji usalama wa milki za ardhi Wilayani Mvomero uliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema kuwa wadau hao wanaifahamu vizuri Wilaya hiyo kuliko wataalam wa wizara hivyo amewataka kutoa maoni, ushauri na mapendekezo chanya ambayo yatasaidia kupunguza au kuondoa kabisa migogoro ya ardhi katika Wilaya hiyo.

“...naomba mtumie nafasi hii kutoa maoni, mapendekezo na mambo muhimu yanayohitajika katika mahitaji yetu halisi kwenye maeneo yetu…” amesema Mkuu wa Wilaya.

Aidha, Mhe. Judith Nguli ametumia mkutano huo kuipongeza na kuishukuru Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuanzisha mradi huo ambao ni tiba ya migogoro ya ardhi ambayo imekuwa ikiipa sifa mbaya Wilaya hiyo. Ameongeza kuwa Vijiji 40 Wilayani humo vimeingizwa katika mpango wa matumizi bora ya ardhi.

Naye, Afisa Mipango miji kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. Paul Kitosi Amesema mradi huo umebuniwa na Serikali ya Awamu ya sita ukiwa na lengo la kusimamia milki za ardhi katika maeneo mbalimbali hapa nchini huku akibainisha kuwa mradi huo unafadhiliwa na mkopo kutoka Benki ya dunia ambapo zaidi ya shilingi bilioni 346 zimekopwa kutekeleza mradi huo. Ameongeza kuwa mradi huo ni wa miaka mitano na ulianza mwaka 2022 na utakamilika 2027.

Aidha, amesema mradi huo umezingatia usawa wa kijinsia huku akisema kuwa mradi huo lengo lake kuu ni kupanga, kupima na kumilikisha viwanja milioni mbili mijini na vijijini hapa nchini.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Bunduki Mhe. Prosper Mkunule ameishukuru Serikali ya awamu ya sita pamoja na Mkuu wa Wilaya kwa kuwa msikivu kwa wananchi wa Wilaya hiyo, aidha amesema mradi huo ni muhimu katika Wilaya hiyo kwani utaupa heshima Wilaya kwa kuwa migogoro ya ardhi itapungua au kuisha kabisa.

Mkutano huo wa wadau wa ardhi unaenda sambamba na kauli mbiu isemayo “usawa wa kijinsia katika umiliki wa ardhi kwa ustawi wa jamii”.


MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.