• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WASISITIZWA KUWA MAKINI KATIKA UANDIKISHAJI WA MAJINA YA WAPIGA KURA

Posted on: February 27th, 2025

Waandikishaji wasaidizi na waendeshaji wa vifaa vya bayometriki katika ngazi ya kituo wamesisitizwa kuwa makini katika uandishi wa majina ya wananchi kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ili kuepuka makosa yanayoweza kuathiri haki ya raia kushiriki katika uchaguzi.

Msisitizo huo umetolewa leo Februari 27, 2025 na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Balozi Omar Ramadhani Mapuri wakati wa mafunzo ya waandikishaji hao, yaliyofanyika katika ukumbi wa Prof. Kuzilwa uliopo Kata ya Mzumbe.

Mhe. Balozi Mapuri ameeleza kuwa usahihi wa majina ni muhimu katika kuhakikisha kuwa kila mpiga kura anaweza kutumia haki yake ya kikatiba bila vikwazo.

"...muhakikishe kwamba majina mnayaandika kwa usahihi na hilo ni muhimu sana sana..." amesisitiza Mhe. Balozi Omar Ramadhani Mapuri.

Sambamba na hilo, Mjumbe huyo amewakumbusha waandikishaji hao kuwa na ushirikiano na mawakala wa vyama vya siasa akibainisha kuwa mawakala hao watasaidia kutambua wakazi halisi wa maeneo yao.

Naye, Afisa Muandikishaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura Jimbo la Mvomero Bi. Mary Kayowa amesema kuwa Jimbo hilo linajumla ya vituo 348 huku akibainisha kuwa washiriki waliopatiwa mafunzo hayo kwa ni 816, ambapo washiriki 408 ni waendesha vifaa vya Bayometriki na 408 ni waandishi.

Ameongeza kuwa washiriki wa mafunzo hayo wamefundishwa mada mbalimbali ambazo zitasaidia katika utekelezaji wa zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu wapiga kura ambalo linataanza rasmi kuanzia tarehe 1 Machi hadi Machi 7 2025.

Mafunzo haya ni sehemu ya maandalizi ya kuhakikisha kuwa mchakato wa uandikishaji wa wapiga kura unafanyika kwa uwazi, usahihi na kwa kuzingatia taratibu zote za uchaguzi.

Zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura linaambatana na kaulimbiu isemayo "Kujiandikisha kuwa mpiga kura ni msingi wa uchaguzi bora"

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.