• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

VIKUNDI VYAHIMIZWA KUCHANGAMKIA MIKOPO YA 10%

Posted on: August 8th, 2024

Waziri Mkuu mstaafu Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda amevitaka vikundi mbalimbali vya Vijana, akina mama na makundi maalum kuchangamkia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kupitia Halmashauri hapa nchini kwa lengo la kukuza mitaji yao pamoja na kuongeza uzalishaji wenye tija.


Mhe. Pinda amesema hayo Agosti 8, mwaka huu kwenye kilele cha Maonesho ya Nane nane Kanda ya Mashariki 2024 yaliyofanyika katika viwanja vya Mwl. Nyerere vilivyopo katika Manispaa ya Morogoro.


Waziri Mkuu huyo Mstaafu amebainisha wakati akitembelea mabanda amekuta vikundi vingi vinajihusisha na kilimo, ufugaji na uvuvi hivyo, amezitaka Halmashauri kuviwezesha vikundi hivyo kupata mikopo hiyo ili kuongeza mitaji yao.


"... tumevikuta vikundi viko hali ya juu kiuchumi lakini vimetokana na mfuko wa 10% na vingine vinapaswa kuchukua kutekeleza majukumu yao, Wakurugenzi wa Halmashauri waliangalie hilo..." amesema Mhe. Mizengo Pinda.


Aidha, Mhe. Pinda amesema Wakurugenzi wa Halmashauri wanatakiwa kuibua vikundi vitakavyonufaika kutokana na mikopo hiyo na ambavyo vitakuwa rahisi kuvifuatilia ili kuendana na kasi ya kukua kwa teknolojia katika uzalishaji wa mazao ya Kilimo, mifugo na uvuvi.


Sambamba na hilo, Waziri Mkuu huyo Mstaafu amesema sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi zimesaidia kupunguza tatizo la ajira kwa Vijana hapa nchini kwani wamekuwa wakifanya shughuli hizo kama vyanzo vya kujipatia kipato.


Katika hatua nyingine, Mhe. Mizengo Pinda amesisitiza wananchi kutilia mkazo suala la lishe bora ambapo amewataka kula mlo kamili ikiwemo vyakula vya mboga mboga kuepuka matatizo ya kiafya ikiwemo utapiamlo ambao bado ni changamoto kubwa kwa baadhi ya maeneo hapa nchini.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima   amesema kumekuwa na mafanikio makubwa katika ushiriki wa maonesho hayo ya Nane Nane kanda ya mashariki kwa mwaka huu kutokana na kuwepo kwa ubunifu wa teknolojia katika sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi, ambapo yamefanya maonesho hayo kuvutia zaidi.


Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wafugaji na wakulima kuwa wa mfano hapa nchini kwa kutumia teknolojia za kisasa, pamoja na kuishi kwa amani na kuheshimiana huku akiwataka wafugaji kuwa na maeneo yao ya kulishia mifugo ili kuondoa migogoro ya wakulima na wafugaji.


Maonesho ya nanenane hufanyika kila mwaka kuanzia Agosti 1 hadi 8 ambapo mwaka huu yamekuwa na kaulimbiu inayosema " Chagua viongozi bora wa Serikali za mitaa kwa maendeleo endelevu ya Kilimo, mifugo na uvuvi".


MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.