• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

VIKUNDI VILIVYOPOKEA MIKOPO ASILIMIA 10 VYAPATIWA MAFUNZO KUIMARISHA MIRADI

Posted on: February 25th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Februari 25, 2025 imeendesha mafunzo maalum kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu vilivyonufaika na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri kupitia mapato ya ndani. Mafunzo hayo yanalenga kuwaongezea ujuzi wa usimamizi wa miradi ili kuongeza ufanisi, tija na urejeshaji wa mikopo kwa wakati.

Akihitimisha mafunzo hayo, Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya hiyo Bi. Sia Ngao amesema kuwa serikali inatilia mkazo utoaji wa mafunzo haya ili kuhakikisha mikopo inayotolewa inaleta maendeleo kwa wanufaika na jamii kwa ujumla.

Aidha, Afisa Maendeleo ya Jamii amewasisitiza wanufaika wa mikopo hiyo kutumia mikopo hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuhakikisha wanaongeza kipato na kurejesha kwa wakati ili wananchi wengine wapate fursa hiyo.

Mafunzo hayo yamejumuisha mada mbalimbali kama Kilimo bora na Ufugaji wa Kuku na Nguruwe, ufugaji wa samaki, mbinu bora za ujasiriamali, usimamizi wa fedha, upatikanaji wa masoko, na namna ya kurejesha mikopo kwa wakati.

Nao baadhi ya wanufaika wa mafunzo hayo akiwemo Bw. Mido Rashidi mwanakikundi cha Family Group kutoka kata ya Mlali ameeleza kuwa mafunzo hayo yamewapa mwanga zaidi kuhusu kilimo bora chenye tija ambacho kitawawezesha kurejesha mkopo waliochukua.

Kwa upande wake Bi. Farida Emily kutoka kikundi cha Kihanu kilichopo Turiani amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fursa hiyo ya mikopo. Pia, ameishukuru Halmashauri kwa mafunzo hayo ambayo yatawaongezea ujuzi katika ufugaji wa kuku wa nyama.

Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero imesisitiza kuwa itaendelea kutoa mafunzo kama haya kwa wanufaika wa mikopo ili kuhakikisha fedha zinazotolewa zinatumika ipasavyo na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WITO UMETOLEWA KWA WADAU, SERIKALI KUONGEZA JUHUDI KATIKA UTOAJI ELIMU YA HEDHI SALAMA VIJIJINI

    May 28, 2025
  • WAHE. MADIWANI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA WATEMBELEA MVOMERO KUJIFUNZA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI UNAVYOWAKOMBOA WAKULIMA WA KAKAO

    May 24, 2025
  • MVOMERO KUUZA UFUTA KUPITIA STAKABADHI GHALANI KUANZIA MEI 20, 2025

    May 16, 2025
  • MKURUGENZI INEC AWASISITIZA WAANDHISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NGAZI YA KITUO KUZINGATIA MUDA WA KUFUNGUA VITUO VYA KUANDIKISHA WAPIGA KURA

    May 14, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.