• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

VIJIJI 5 MVOMERO KUNUFAIKA NA MRADI WA HEWA UKAA

Posted on: April 30th, 2024

Vijiji 5 Wilayani Mvomero vinatarajia kunufaika na mradi wa kupunguza uzalishaji wa Hewa Ukaa (Kaboni) unaotokana na uharibifu wa misitu ikiwemo ukataji na uchomaji wa misitu hovyo ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Hayo yamebainishwa Aprili 30, 2024 na Meneja wa Uendeshaji kutoka Kampuni ya Village Climate Solution Limited Bw. Aklei Albert wakati wa kikao cha Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango kilicholenga kuwasilisha mapendekezo ya kuidhinisha rasimu ya makubaliano ya kuanzisha, kutekeleza na kugawana gharama na faida ya mradi wa kaboni kati ya Vijiji vya mradi, Halmashauri na Kampuni ya Village Climate Solutions kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.

Bw. Albert amesema Mvomero ni miongoni mwa Wilaya zinazotekeleza mradi wa hewa ya ukaa Mkoani Morogoro ambapo mradi huo unatekelezwa katika hifadhi za misitu ya Vijiji 5 vya Maharaka, Kihondo, Misengele, Sewekipera na Msongozi.

Aidha, ameongeza kuwa lengo la mradi huu ni kuwezesha vijiji vinavyomiliki misitu ya asili kunufaika na misitu yao kupitia biashara ya kuuza hewa ya ukaa yaani kaboni.

Naye, Mwanasheria wa Halmashauri hiyo Bi. Cotrida Komba amesema vijiji vya mradi vinatarajia kupata zaidi ya asilimia 60 kupitia biashara ya hewa ya ukaa. Imeelezwa kuwa kwa mujibu wa taratibu za biashara ya kaboni hapa nchini mikataba ya biashara hiyo inachukua miaka 30 hadi 40 hivyo, Halmashauri hiyo imependekeza iwe kwa kipindi cha miaka 40.

Kwa upande wake Mhe. Christopher Maarifa kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero amelishukuru shirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania (TFCG) kupitia Kampuni ya Village Climate Solution Limited (VCSL) kwa kuleta mradi huo katika Wilaya ya Mvomero na kuahidi kutoa ushirikiano ili kufanikisha mradi huo.


MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.