• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

VIJANA 200 KUNUFAIKA NA MRADI WA KILIMO TIJA

Posted on: April 24th, 2024

Vijana zaidi ya 200 Wilayani Mvomero wanatarajia kunufaika na mradi wa Kilimo Tija unaolenga kutoa elimu ya kilimo kwa vitendo pamoja na kuwawezesha kupata pembejeo za kilimo na ardhi kwa ajili ya kulima ili kuwainua kiuchumi.

Hayo yamebainishwa Aprili 24, 2024 na Mkuu wa Wilaya Mvomero Mhe. Judith Nguli wakati akizindua rasmi mradi wa Kilimo Tija Wilayani humo, zoezi hilo la uzinduzi umefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo.

Mhe. Nguli ameeleza kuwa Mradi huo utawanufaisha vijana 200 kutoka Kata ya Lubungo na maeneo mengine ya Wilaya hiyo ambapo watapatiwa Ardhi, miundombinu ya umwagiliaji pamoja na mikopo ili kuongeza uzalishaji wenye tija kwa mazao ya matango, matikiti maji na mbogamboga.

“...vijana 200 watapata fursa ya kupata uwezeshwaji katika mradi huu kwa maana watapewa ardhi kama ilivyoorodheshwa hapo lakini pia watalima mazao yaliyotajwa kutoka kwenye ekari 100 za SUGECO...” amsema Mkuu wa Wilaya.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya ameipongeza SUGECO (Sokoine University Graduate Entrepreneurs Cooperative) kwa kuunga mkono juhudi za Serikali za kuwainua vijana kwa kuanzisha mradi huo Wilayani humo na kuwataka vijana kuchangamkia fursa hiyo muhimu kwani itanua uchumi wa vijana wa Wilaya hiyo.

Ameongeza kuwa pamoja na mradi kuwanufaisha vijana 200 lakini pia utazalisha ajira 1410 kwa vijana huku akibainisha kuwa jambo hilo linaunga mkono dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuzalisha ajira milioni nane hadi kufikia mwaka 2025.

Naye Mkurugenzi wa SUGECO Bw. Revocatus Kimario ameeleza kuwa mradi huo utatekelezwa katika Kijiji cha Lubungo na utakuwa wa miaka mitatu hadi 2027, walengwa ni vijana kuanzia umri wa miaka 15 hadi 35. Ameongeza kuwa vijana hao watapatiwa ardhi kuanzia nusu ekari hadi ekari tatu, kupatiwa pembejeo za kilimo, mikopo kutoka taasisi za kifedha, kutafutiwa masoko ya uhakika ndani na nje ya nchi pamoja na kutafutiwa ajira.

Nao wanufaika wa mradi huo akiwemo Bw. John Ruanda ameishukuru Serikali ya Awamu ya sita kwa kuweka mazingira mazuri kwa wadau wa maendeleo ambapo imesaidia kupatikana fursa kama zinazotolewa na SUGECO, pia amewataka Vijana kuipokea fursa hiyo kwa mikono miwili ili waweze kujikwamua kiuchumi.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.