• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

UVCCM MZUMBE YAFANYA DUA KUMUOMBEA RAIS SAMIA, DC NGULI AWATAKA VIJANA WASIPOTOSHWE

Posted on: February 1st, 2025

Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Tawi la chuo kikuu Mzumbe umefanya dua na maombi maalum ya kuliombea Taifa pamoja na kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi wakiombewa afya njema, hekima na uongozi wenye mafanikio kwa ajili ya maendeleo ya taifa kuelekea uchaguzi Mkuu ambao unatarajiwa kufanyika mwaka huu.

Dua hiyo imefanyika Februari Mosi, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Shule ya Sekondari Mzumbe, hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi wa Chama, Serikali, wanachama wa CCM, wanachuo na Wananchi.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mhe. Judith Nguli, ambaye alikuwa mgeni rasmi wa hafla hiyo amewataka vijana kuwa makini na kupinga upotoshaji unaoenezwa na watu wenye nia ovu dhidi ya maendeleo ya taifa, huku akisisitiza umuhimu wa vijana kushiriki katika ujenzi wa nchi kwa kushikamana na kuunga mkono juhudi za serikali.

"...sasa kuna watu wanapotosha hapa anaingia kwenye kundi la vijana hili ndo analijaza sumu badala ya kumuonesha njia..." amesema Mkuu wa Wilaya.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma bora za msingi ikiwemo za Afya, Elimu, Maji na umeme pamoja na kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji ili kuwavuta wawekezaji walete fursa za ajira kwa vijana.

Aidha, amewashukuru Viongozi wa dini Wilayani humo kwa kazi kubwa ya kuliombea taifa pamoja na viongozi wengine usiku na mchana ili amani na utulivu viendelee kudumishwa huku akibainisha kuwa sala na dua ni muhimu katika kuliongoza taifa.

Naye Mwenyekiti wa UVCCM Seneti Mkoa wa Morogoro ndg. Powell Maruma amesema dua hiyo ni ishara ya mshikamano wao na serikali katika kuhakikisha maendeleo yanapatikana kwa amani na utulivu. Aidha, amesisitiza kuwa vijana wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kulinda amani, kushiriki shughuli za maendeleo na kuhamasisha uzalendo.

Kwa upande wake Shekhe wa Kata ya Mzumbe Shekhe Suleiman Mzee amesema ili Taifa liwe salama ni lazima wananchi pia wawe salama kwa kuyaacha matendo yote ambayo Mwenyezi Mungu ameyakataza na kuyatenda yale ambayo yanatakiwa kufanywa.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KUMULIKA MIRADI YA MAENDELEO 7 YENYE THAMANI YA TSH. 1.06 WILAYANI MVOMRO

    April 13, 2025
  • DC MVOMERO AAGIZA SHULE SHIKIZI MINGO ISAJILIWE, IPOKEE WANAFUNZI JANUARI 2025

    March 27, 2025
  • KUU MVOMERO YAKISHUKURU KIWANDA CHA SUKARI MTIBWA KWA KUSAIDIA WANANCHI KURUDISHA MTO KWENYE MKONDO WAKE

    March 19, 2025
  • RAS MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA "JISOMESHE NA MKARAFUU" KUWAWEZESHA WANAFUNZI KIUCHUMI

    March 14, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.