• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

UMITASHUMTA MVOMERO YAPAMBAMOTO, DED LINNO ASISITIZA NIDHAMU

Posted on: May 27th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mwl. Linno Mwageni amewataka Wanafunzi wanao shiriki mashindano ya michezo kwa shule za Msingi – UMITASHUMTA Wilayani Mvomero kuwa na nidhamu ili waweze kupata mafanikio katika mashindano hayo.

Mwl. Mwageni ametoa wito huo leo Mei 26, 2024 wakati akifungua mashindano ya UMITASHUMTA kwa ngazi ya Wilaya ambayo yanaendelea katika viwanja vya michezo vya Chuo Kikuu Mzumbe .

Mkurugenzi huyo amesema nidhamu na bidii humfanya mtu kuyafikia malengo yake ambayo amejiwekea hivyo akawasisitiza washiriki hao ili waweze kufika mbali katika sekta ya michezo.

“...jamani mkishindwa kuleta vikombe vyote mkaniletee kikombe cha nidhamu kwa sababu hicho hakihitaji kuvuja jasho wala nini kinachotakiwa kila kitu mfanye kwa nidhamu...” amesema Mwl. Mwageni.

Aidha amewataka washiriki kujituma katika mashindano hayo na kwamba wasiende kushiriki bali wakashindane ili wapate nafasi katika ngazi zote kuanzia ya Wilaya, Mkoa na Taifa kwa ujumla.

Katika hatua nyingine, Mwl. Mwageni amewashukuru na kuwapongeza walimu ambao wamewatoa wanafunzi wao ili washiriki UMITASHUMTA huku akiwataka kuwa walezi bora wa wanafunzi hao.

Kwa upande wake Afisa michezo wa Halmashauri hiyo Bw. Charles Kajiru amebainisha kuwa kambi hiyo ni ya siku tatu kuanzia leo Mei 26 hadi Mei 28 na michezo inayoshindanishwa ni pamoja na mpira wa miguu, mikono, wavu, kikapu, mpira wa pete na kwaya. Ameongeza kuwa timu ya Wilaya itakuwa na wachezaji 88 hadi 90, walimu 10 pamoja na viongozi wengine.

Nao washiriki wa michezo hiyo akiwemo Thomas Ventus amesema timu yao ya mpira wa wavu ilifanya vizuri katika mashindano ya UMITASHUMTA 2023 na kwamba anaamini na mwaka huu watafanya vizuri zaidi.

Mashindano ya UMITASHUMTA 2024 yanaenda sambamba na kaulimbiu isemayo “Miaka 50 ya UMITASHUMTA, Tunajivunia mafanikio katika Sekta ya Elimu, Michezo na Sanaa, hima mtanzania shiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024”

MWISHO.











Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.