• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

"TUNATAKA KURUDISHA HADHI YA MOROGORO YA VIWANDA" - RAIS SAMIA

Posted on: August 6th, 2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali yake imepanga kurejesha hadhi ya Mkoa wa Morogoro kuwa wa Viwanda kama ilivyokuwa awali ambapo Mkoa huo ulikuwa na Viwanda vingi.

Dkt. Samia amebainisha hayo leo Agosti 06, 2024 wakati akizungumza na wananchi wa Mkoa huo kwenye mkutano  wa hadhara akihitimisha ziara yake ya kikazi Mkoani humo.

Rais Samia amesema lengo la kurejesha Viwanda hivyo ni kukuza uchumi wa Mkoa pamoja na kuongeza ajira kwa vijana wa Mkoa na Taifa kwa ujumla.

"...Tunataka kurudisha hadhi ya Morogoro ya Viwanda..." amesema Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aidha, Dkt. Samia amesema ameshatoa maelekezo kwa Waziri wa Viwanda na Biashara kuhakikisha kuwa viwanda vilivyopo havifi na vile vilivyokufa vinafufuliwa ili vianze kuzalisha akitolea mfano Kiwanda cha Vipuri cha Mang'ula na Kiwanda cha mafuta ya kupikia.

Sambamba na hilo, amesema uwepo wa Reli ya SGR na umeme wa uhakika unafanya Mkoa huo kuwa sehemu sahihi ya uwekezaji huku akiwataka viongozi na wananchi kuacha mivutano badala yake watenge maeneo ya uwekezaji ili kupata wawekezaji wengi.

Naye, Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe amebainisha kuwa kuwa Mkoa wa Morogoro hususan Manispaa ya Morogoro ni kitovu cha viwanda vingi vinavyochakata bidhaa za kilimo. Waziri Bashe ameongeza kuwa kupitia kiwanda cha Tumbaku na Sigara watu 12000 wataajiliwa hadi kufikia Juni 2025.Waziri huyo wa Kilimo ameeleza kuwa Serikali inatarajia kufufua kiwanda cha Morogoro Farmers ambacho kitazalisha nyuzi za kufungia tumbaku ambazo Serikali huziagiza kutoka nje ya nchi kwa gharama kubwa hivyo hadi kufikia Disemba 2025 kiwanda hicho kitakuwa kimefufuliwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema Mkoa huo ni Mkoa wa Kilimo huku akibainisha kuwa hata viwanda vilivyopo vinachakata bidhaa zitokanazo na mazao ya kilimo. Aidha, ameongeza kuwa upatikanaji wa umeme umerahisisha uzalishaji katika  viwanda vya Mkoa huo.
Rais Samia anatarajia kuhitimisha ziara yake Mkoani Morogoro  kwa kuzindua Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.