• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

TFS YAPONGEZWA KUBORESHA HUDUMA ZA JAMII

Posted on: July 1st, 2024


Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amewapongeza  Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania - TFS Wilayani humo kwa kuunga mkono Serikali kwa kuboresha huduma za jamii zikiwemo elimu, Afya, maji na huduma zingine muhimu kwani kwa kufanya hivyo kunasaidia jamii kutatua ama kumaliza kabisa changamoto zake.

Mhe. Nguli ametoa pongezi hizo Julai Mosi, 2024 wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa vya ujenzi kwa ajili ya umaliziaji wa Ofisi ya Serikali ya Kijiji Cha Wami Sokoine na ukarabati wa shule iliyofanyika katika Shule ya Msingi Sokoine.

Mkuu huyo wa Wilaya amebainisha kuwa kwa sasa kuna uhitaji mkubwa wa madarasa na madawati kwa sababu ya  ongezeko kubwa la watoto katika shule mbalimbali kutokana na Serikali kutekeleza Sera ya Elimu bila malipo, hivyo amipongeza TFS kwa kujitoa kuboresha miundombinu ya elimu pamoja na huduma nyingine katika Wilaya hiyo.

*"...mimi niwapongeze sana TFS mmekuwa mfano mzuri kwa sababu kila mwaka mnafanya haya..."* amesema Mkuu wa Wilaya.

Aidha, amesema kuwa Taasisi zinazojitoa kwa ajili ya kuboresha huduma za jamii zinajenga mahusiano mazuri na jamii husika hivyo kurahisisha baadhi ya shughuli za taasisi hizo.

Sambamba na hilo Mhe. Nguli ametoa rai kwa taasisi nyingine kushiriki katika zoezi la kuboresha huduma za jamii kwani sheria na miongozo ya nchi zinahimiza taasisi kuhakikisha kuwa  zinarudisha huduma kwa jamii.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya amewataka wazazi kufuatilia mienendo ya watoto wao ili kuwalinda dhidi ya vitendo vya ukatili ambavyo vimekuwa tishio kwa usalama wa watoto.

Naye, Afisa Muhifadhi wa Shamba la Miti Morogoro Bw. Mohammed Kiyangi amesema TFS kupitia Ofisi ya hifadhi ya shamba la miti Morogoro imekuwa na utaratibu wa kuchangia shughuli za maendeleo kwa jamii zinazozunguka maeneo ya hifadhi.

Ameongeza kuwa hifadhi ilipokea barua kutoka Serikali ya Kijiji cha Wami Sokoine iliyobainisha  mahitaji muhimu ya vifaa vya ujenzi kwa ajili ya shule pamoja na umaliziaji wa ofisi ya Serikali ya Kijiji. Hata hivyo, Afisa Muhifadhi huyo amebainisha changamoto zinazoikabili hifadhi ya shamba la miti Morogoro ikiwa ni pamoja na ongezeko la mifugo katika hifadhi ambayo imekuwa ikikwamisha na  kurudisha nyuma juhudi za uhifadhi wa msitu.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Sokoine Mwl. Tambwe Mavumila amesema kuwa shule hiyo inakabiliwa na upungufu na uchakavu wa vyumba vya madarasa ambapo kwa sasa shule hiyo ina madarasa 11 kati ya 33 yanayohitajika huku ikiwa na wanafunzi 1446. Aidha, ameshukuru kwa vifaa hivyo ambapo anaamini itapunguza changamoto ya madarasa huku akibainisha kuwa wanafunzi ni wengi wanakaa chini kutokana na uchache wa madarasa na madawati.

Katika hafla hiyo vifaa vilivyokabidhiwa ni pamoja na mbao 90 saruji mifuko 88, gypsum bodi vipande 25 na gypsum powder mifuko mitatu vifaa vyote vinathamani ya shilingi 3,002,000.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.