• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

TAASISI ZA KIFEDHA ZINAZOKIUKA MISINGI YA LESENI KUCHUKULIWA HATUA

Posted on: August 22nd, 2024

Wananchi wametakiwa kufichua Taasisi zinazotoa huduma za kifedha hususan zinazokiuka misingi ya Leseni katika utoaji wa mikopo kandamizi (mikopo kausha damu) kwa wateja wake pamoja na kuwafanyia vitendo vya uzalilishaji ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya taasisi hizo.


Wito huo umetolewa Agosti 22, 2024 na Afisa Msimamizi wa Fedha kutoka Wizara ya Fedha Bw. Jackson Mushumba wakati wa Mafunzo ya usimamizi wa fedha yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Community Centre uliopo Kata ya Mtibwa Wilayani Mvomero.


Bw. Jackson amesema kuwa Taasisi zote zitakazo bainika kukiuka misingi ya utoaji mikopo kama ilivyoelekezwa na Benki Kuu ya Tanzania chini ya Wizara ya Fedha zitachukuliwa hatua ikiwemo kufutiwa leseni huku akiwataka wananchi kutoa taarifa kwa viongozi kuanzia ngazi ya Vijiji hadi Wilaya pindi wanaposhuhudia ukiukwaji wa misingi ya leseni.


“...sheria ipo wazi ni adhabu gani kwa hawa watoa huduma wanaokiuka taratibu, adhabu moja wapo ni pamoja na kufutiwa leseni zao...” amesema Bw. Jackson.


Aidha, amesema Wizara imeboresha mfumo wa kufichua taasisi zinazotoa huduma ndogo za kifedha hususan zinazotoa mikopo kausha damu ambapo taarifa za mwananchi atakayebainisha taasisi hizo zitalindwa.


Katika hatua nyingine, Afisa huyo amewataka wananchi kusajili vikundi vyao ili kuwa na usalama wa fedha zao katika vikundi hivyo.


Naye Bi. Grace Samwel ambaye ni Afisa Usimamizi wa Fedha (Wizara ya Fedha) amewataka wananchi kuyaelewa masharti ya mikopo kabla ya kuchukua mikopo hiyo. Pia, amezitaka taasisi zinazotoa huduma za kifedha kuainisha na kuweka wazi masharti na taratibu za kupata mikopo katika taasisi zao.


Kwa upande wao wananchi akiwemo Bi. Latifa Japhari wakati akichangia mada zilizowasilishwa na maafisa hao, amewashauri wananchi wengine kuwa na tabia ya udadisi ili kubaini kama wanatendewa haki pindi wanapoenda kuchukua mikopo kwenye taasisi zinazotoa huduma za kifedha.


Ikumbukwe kuwa sharia ya mikopo kwa taasisi ndogo zinazotoa huduma za kifedha imeelekeza taasisi hizo kutoza riba isiyozidi asilimia 3.5 katika mikopo inayotoa.


MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.