• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

SKAUTI MVOMERO WAADHIMISHA KUMBUKIZI YA KUZALIWA MWANZILISHI WA SKAUTI DUNIANI KWA KUFANYA USAFI SEHEMU ZA JAMII

Posted on: February 22nd, 2025

Skauti Wilayani Mvomero wameadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwa mwanzilishi wa Harakati za Skauti Duniani, Sir Robert Stephenson Smyth Baden Powell, kwa kufanya shughuli za usafi katika maeneo mbalimbali ya jamii.

Maadhimisho hayo yamefanyika leo Februari 22, 2025 katika mazingira ya mshikamano na huduma kwa jamii, ambapo skauti wameshiriki kusafisha Soko la Dakawa, Kituo cha Afya Dakawa,  Kituo cha Polisi Wilaya ya Mvomero na kwenye mifereji ya  barabara, lengo ni kuonesha dhamira yao ya utunzaji wa mazingira kwa vitendo.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Kamishna wa Skauti Wilaya ya Mvomero,  Mwl. Charles Kajiru amesema kuwa lengo la shughuli hiyo ni kuendeleza maadili ya skauti ya kuwajibika kwa jamii na kutunza mazingira.

Aidha, ameongeza kuwa madhumuni makubwa ni kuhakikisha kuwa vijana wa skauti wanakuwa wasafi kwenye maeneo yao ya nyumbani pamoja na kuifundisha jamii juu ya umuhimu wa kutunza mazingira. Pia, ametoa wito kwa wananchi Wilayani humo kuwa na tabia ya kufanya usafi katika maeneo yao.

Sambamba na hilo, Kamishna huyo wa Skauti amewataka vijana kufikisha ujumbe kwa wazazi wao ili waweze kujitokeza kwa wingi wakati wa zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ambapo kwa Wilaya ya Mvomero zoezi hilo linatarajiwa kuanza tarehe 01-07 Machi, 2025.

Nao baadhi ya Vijana wa Skauti walioshiriki zoezi hilo akiwemo Elias kutokea kata ya Dakawa amesema zoezi hilo ni sehemu ya kuenzi maneno ya Mwanzilishi wa Skauti duniani ambapo alisema "acha dunia yangu ikiwa safi na bora".

Maadhimisho ya kumbukizi ya kuzaliwa kwa Sir Robert  Stephenson Smyth Baden Powell huadhimishwa kila mwaka tarehe 22 Februari na skauti kote duniani kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii, ikiwa ni sehemu ya kuenzi mchango wake katika kuanzisha na kuendeleza harakati za skauti duniani.

Kaulimbiu ya kumbukizi ya kuzaliwa kwa Mwanzilishi huyo wa Skauti duniani inasema "Skauti toa maoni ya Dira ya Taifa 2050, Shiriki uchaguzi Mkuu 2025"

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.