• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

SIKU YA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA YAADHIMISHWA MVOMERO

Posted on: July 25th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli ameongoza mamia ya viongozi  wa Serikali pamoja na wananchi katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mashujaa Tanzania yaliyofanyika katika Kijiji cha Mvomero, Kata ya Mvomero tarehe 24.07.2023.

Katika maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya aliwakumbusha wananchi umuhimu wa wao kujitoa kwa ajili ya taifa lao na kuwa wazalendo kwa nchi yao na kuiga mfano wa mashujaa waliolipigania taifa  mfano akiwa Koplo Fokas Emmanuel kutoka Wilaya ya Mvomero.

“Leo tunaadhimisha siku hii Kiwilaya. Naomba tuwaunge mkono mashujaa wetu. Kwa sisi sasa hivi, tulipiganie taifa kwa matendo. Tunahitaji wazalendo kwenye Wilaya yetu kama Koplo Fokas Emmanuel. Tuwaepuke walio na nia mbaya na Wilaya yetu.”aliongeza Mkuu wa Wilaya.

Kwa upande mwingine, mmoja wa askari aliyepigana vita ambaye pia ni mwananchi wa Wilaya ya Mvomero Kapteni Mstaafu Kiloko mwenye umri wa miaka 77 amewaasa vijana kuwa na umoja na kutoogopa kujiunga na jeshi kwani si gumu kama wanavyohadithiwa.

“Wakati wa Vita ya Kagera, Watanzania wote walishiriki kumuondoa Nduli Amin Dada kwa namna yao. Kila mmoja alichangia alichonacho. Wengine kuku, mchele yote katika uzalendo wa nchi yao” aliongeza Kapteni Mstaafu Kiloko.

Akitoa salamu kwa niaba ya Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Yusuph Makunja aliwataka wananchi kuwa na imani na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwani kupitia yeye ameendelea kuwaletea Wana-Mvomero viongozi bora na wachapakazi mfano akiwa Mkuu wa Wilaya Mhe. Judith Nguli.

Katika Maadhimisho hayo, viongozi Serikali, dini na wanajeshi wastaafu waliweka zana mbalimbali za jadi kwenye mnara wa Kumbukumbu wa mmoja wa mashujaa Koplo Fokas Emmanuel ikiwa ni kuthamini jitihada na mchango wa askari waliopambana kwenye vita ya ukombozi wa taifa. Zana zilizosimikwa ni pamoja na mkuki, ngao,mshale, shoka na mashada ya maua kama ishara ya kuwaenzi mashujaa wa Tanzania.

Maadhimisho hayo pia yaliendana na kufanya usafi katika kituo cha Afya Mvomero ambapo viongozi, watumishi wa kituo hiko pamoja na wananchi walijumuika pamoja kufanya usafi eneo linalozunguka kituo hiko.

Eneo la Mvomero kuna mnara wa mmoja wa askari mashujaa aliyeshiriki kwenye vita ya ukombozi wa nchi Koplo Fokas Emmanuel aliyefariki dunia wakati akilipigania taifa vitani tarehe 10.4.1979.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.