• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

SHIRIKA LA SAWA LAPONGEZWA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA ELIMU

Posted on: October 18th, 2024

Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero imepongeza juhudi za Shirika la SAWA WANAWAKE TANZANIA katika kuboresha miundombinu ya elimu Wilayani humo, Shirika hilo limekuwa likifanya kazi kwa karibu na serikali na jamii katika kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi kwa kujenga na kukarabati madarasa, pamoja na kuweka vifaa vya kisasa katika shule za msingi na sekondari pamoja na miundombinu ya maji.

Akizungumza Oktoba 18, 2024 wakati wa hafla ya makabidhiano ya mradi wa ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa, vyoo na kisima cha maji katika shule ya Msingi Makuture, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mhe.  Yusuf Makunja ameeleza kuwa juhudi hizi zinalenga kuongeza kiwango cha elimu na kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata mazingira bora ya kusomea.

 "Mchango wa Shirika la SAWA unasaidia sana kupunguza changamoto zinazowakabili wanafunzi katika upatikanaji wa elimu bora." amesema Mhe. Makunja.

Aidha, amebainisha kuwa shule hiyo ilikuwa ikikabiliwa na ukosefu wa maji safi hivyo kusababisha wanafunzi kutumia muda mwingi kutafuta maji kuliko masomo, pia amesema uhaba wa madarasa ulipelekea shule hiyo kuwa na vipindi viwili vya masomo yaani wanasoma asubuhi wengine mchana.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la SAWA Bi. Hellen Nkalang'ango ameeleza kuwa lengo lao ni kusaidia jamii za kipato cha chini kupata fursa sawa katika elimu na kuongeza kiwango cha ufaulu huku akisisitiza kuwa shirika hilo litaendelea kujitolea katika kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuboresha sekta ya elimu nchini.

Kwa upande wao Wananchi wa Kitongoji cha Makuture ambao wanafaidika na mradi wa Shirika la SAWA wameeleza kuwa, maboresho hayo yameleta mabadiliko makubwa katika mazingira ya shule na hamasa kwa wanafunzi kuzingatia masomo.

Pamoja na mradi huo Shirika la SAWA limekabidhi mradi wa kisima cha maji, madarasa mawili, ofisi moja na vyoo katika shule msingi shikizi ya Mtakuja.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.