• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

SHILINGI 185,298,000 ZIMELIPWA KWA WALENGWA 6130 MVOMERO

Posted on: November 7th, 2024

Serikali kupitia Mpango wa kunusuru Kaya Maskini – TASAF imetoa kiasi cha shilingi 185,298, 000 kwa ajili ya kuwalipa walengwa 6130 wa mpango huo Wilayani Mvomero ambapo malipo hayo ni dirisha la mwezi Julai na Agosti, 2024.

Hayo yamebainishwa Novemba 07, 2024 na Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mahija Mdoe wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii ikiwa zoezi la ulipaji likiendelea kwa Vijiji 130 vya Wilaya hiyo.

Mratiu huyo amesema dirisha hilo la malipo kitaifa lilifunguliwa rasmi tarehe 28 Oktoba, 2024 mwisho wake ni Novemba 7, 2024 huku akibainisha kuwa katika Hamashauri ya Wilaya ya Mvomero ina walengwa 6130 ambapo kati yao walengwa 3593 wamepokea fedha tasilimu kiasi cha shilingi 108,832,000 na kiasi cha shilingi 76, 466,000 zimelipwa kwa walengwa 2537 kwa njia ya mtandao yaani kwa njia ya benki na mitandao ya simu.

Aidha, ameongeza kuwa Serikali inandelea kuhamasisha walengwa ambao bado wanapokea fedha tasilimu kuunganishwa kwenye mtandao ili waweze kupokea fedha zao kupitia benki au mitandao ya simu kwani kwa njia ya mtandao walengwa wanapakea fedha zao mapema ukilinganisha na wanaopokea fedha tasilimu.

Akielezea faida za malipo ya walengwa kwa njia ya mtandao Afisa Ufuatiiaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Bw. Mweta Kharidi amesema njia hiyo inafaida kwa Serikali na kwa walengwa wenyewe. Kwa upande wa Serikali inasaidia kupunguza gharama za uendeshaji wa mradi ikiwemo kulipa askari, kulipa kamati za usimamizi ngazi ya jamii (CMC).

Nao baadhi ya wanufaika wa mpango huo akiwemo Bi. Fadhila Shomari Mkazi wa Kijiji cha Mbogo ameishukuru Serikali kwa kuanzisha mradi huo ambao umemsaidia kujenga nyumba ya chumba kimoja.

Nae Bw. Abdallah Matuwa amesema kupitia TASAF ameweza kujenga nyumba na amenunua baiskeri hivyo ameishukuru Serikali kuwawezesha kiuchumi.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.