• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

RUWASA MVOMERO YAPONGEZWA KWA KUTATUA CHANGAMOTO YA UHABA WA MAJI KATA YA MANGAE

Posted on: September 29th, 2024

Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Morogoro imeipongeza Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini - RUWASA Wilayani Mvomero kwa jitihada zake za kutatua changamoto ya uhaba wa maji kwa Wananchi wa Kata ya Mangae.

Pongezi hizo zimetolewa Septemba 29, 2024 na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Morogoro, Ndugu Solomon Kasaba, wakati wa ziara ya Kamati hiyo ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM Wilayani Mvomero.

Ndugu Kasaba amesema RUWASA imeleta suluhisho la kudumu kwa changamoto za maji zinazo wakabili wakazi wa Kata ya Mangae kwa muda mrefu. Amebainisha kuwa juhudi hizo zina akisi dhamira ya dhati ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kumtua mama ndoo kwa kuwasogezea huduma ya maji karibu na maeneo yao.

"...kwa uamuzi mliouchukua kabla ya mradi kukamilika kupunguza makali watu waanze kupata maji, tunawapongeza sana..." amesema Ndugu Kasaba.

Aidha, Katibu huyo wa CCM amewataka wananchi waendelee kuunga mkono juhudi za serikali na taasisi zake katika kutatua changamoto zinazowakabili, huku akisisitiza wananchi kuutunza mradi huo ili udumu akibainisha kuwa CCM itaendelea kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa miradi mbalimbali ili kuhakikisha mafanikio yanafikiwa kwa wakati na kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Meneja wa RUWASA Wilaya ya Mvomero Mhandisi Mlenge amesema mradi huo umefikia asilimia 78 huku akisema kuwa kazi zilizofanyika ni pamoja na ujenzi wa vituo 19 vya kuchotea maji, ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilometa 14. Aidha amesema mradi huo unagharimu kiasi cha milioni 643.

Nao wananchi wa Kata ya Mangae wameishukuru Serikali kwa mradi huo wa maji ambao utawapunguzia adha ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma hiyo katika maeneo mengine.

Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Morogoro inaendelea na ziara zake katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyoainishwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020.

MWISO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.