• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

RAS MOROGORO ARIDHISHWA NA MRADI WA UBORESHAJI MISITU, AMUAGIZA DED MVOMERO KUSHUGHULIKIA SUALA LA HATI

Posted on: July 17th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Mussa Ali Mussa ameonesha kuridhishwa na mradi wa Uboreshaji wa Misitu unaotekelezwa chini ya shirika la PAMS Foundation katika Kata ya Pemba

Wilayani Mvomero, huku akimuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kushughulikia suala la upatikanaji wa hatimiliki za kimila kwa wananchi bila kujali kama ni wanufaika wa mradi huo.

Dkt. Mussa ametoa agizo hilo Julai 17, 2025, alipotembelea Kitongoji cha Disanga kwa lengo la kukagua maendeleo ya mradi huo unaolenga kurudisha uoto wa asili kupitia upandaji wa miti.

Katibu Tawala huyo amebainisha kuwa mradi huo umeonesha manufaa kwa wakazi wa eneo ambalo mradi unatekelezwa kutokana na kuwapatia fursa mbalimbali ikiwemo ajira za muda, elimu ya uzalishaji wenye tija pamoja na elimu ya uhifadhi wa misitu. Aidha, amelipongeza shirika PAMS kwa kuja na wazo la mradi huo.


"...mimi niwashukuru sana hawa wenzetu wa PAMS kwa kuleta huu mradi wa kuhifadhi misitu...niseme wamefanya kazi nzuri...agizo langu mimi hata kwa wale ambao hawapo katika mpango huo wa PAMS na wao ufanye mpango wapewe hati zao za kimila kutokana na maeneo waliyokuwa nayo..." amesema Dkt. Mussa.


Aidha, amewapongeza wananchi kwa kukubali na kuupokea mradi huo ambao una manufaa si tu kwenye mazingira bali na kiuchumi pia huku akiwataka kuendelea kutoa ushirikiano.


Kwa upande wake, Msimamizi wa mradi huo kutoka shirika hilo Bw...amesema kuwa jumla ya mashamba 538 ya wanufaika yenye jumla ya ekari 1560 yamepimwa na kuingizwa kwenye mradi huo, pia amebainisha kuwa kupitia mradi huo wanufaika 347 wamelipwa kiasi cha shilingi milioni 250 ikiwa ni fedha za ushiriki katika mradi pamoja na fidia ya mazao ya kudumu kwa mashamba yaliyo katika eneo la mradi.


Ameongeza kuwa hadi sasa jumla ya miche ya miti 11000 imezalishwa ambapo miche 6000 imetolewa kwa Halmashauri na miche 5000 imetolewa kwa taasisi mbalimbali zilizopo katika Kata ya Pemba.


Wananchi wamenufaika wa mradi huo wamesema PAMS imekuwa mkombozi wa kiuchumi kwa sasa kwani baadhi yao wamepata ajira, imerahisisha upatikanaji wa hati za kimila

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MZUMBE UNIVERSITY YAUNGA MKONO KAMPENI YA MAMA SAMIA LEGAL AID, YAKABIDHI VITABU 400 VYA SHERIA

    July 21, 2025
  • PAMS FOUNDATION YAPONGEZWA KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    July 19, 2025
  • RAS MOROGORO ARIDHISHWA NA MRADI WA UBORESHAJI MISITU, AMUAGIZA DED MVOMERO KUSHUGHULIKIA SUALA LA HATI

    July 17, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUTOGOMEA MIRADI YENYE TIJA KWENYE UCHUMI

    July 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.