• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

RAS MOROGORO AFUNGUA MAFUNZO KWA WAANDIKISHAJI, AWATAKA KUFIKA VITUONI KWA WAKATI

Posted on: October 8th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro ambaye pia ni Msimamizi wa Uchaguzi Mkoani humo Dkt. Mussa Ali Mussa ametoa wito kwa waandikishaji wa wapiga kura wa Serikali za Mitaa kuhakikisha wanawahi kufika vituoni kwa wakati ili kuimarisha mchakato wa uandikishaji wa wapiga kura kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakao fanyika tarehe 27 Novemba, 2024.

Dkt. Mussa ametoa wito huo Oktoba 08, 2024 wakati wa Semina ya Waandikishaji wa Wapiga kura kutoka Tarafa za Mgeta na Mlali iliyofanyika katika ukumbi wa shule ya Sekondari Mzumbe.

Katibu Tawala huyo amesisitiza kuwa hatua hiyo itasaidia kurahisisha zoezi zima la kuandikisha wapiga kura kwa ufanisi, kuhakikisha kuwa hakuna ucheleweshaji unaoweza kuathiri zoezi hilo muhimu kwa demokrasia.

"...neno langu la kwanza ninaloliona sisi tufike katika vituo mapema..." amesema Dkt. Mussa

Ameongeza kuwa kufika mapema kutasaidia kuepusha msongamano katika vituo na kuleta usawa kwa wapiga kura wote wanaotaka kujiandikisha na kupiga kura.

Pamoja na hayo Dkt. Mussa amewasisitiza waandikishaji hao kuhakikisha kuwa vifaa vinavyohitajika katika zoezi hilo la uandikishaji vinakuwepo katika vituo vyao kwa idadi inayohitajika, amewataka kuwa wasiri na  kuzingatia taratibu ili kuhakikisha zoezi la uchaguzi linakamilika kwa mafanikio. Pia amewataka kuwa na lugha nzuri kwa wananchi watakaofika vituoni kujiandikisha.

Naye, Msimamizi msaidizi wa Uchaguzi Mkoa wa Morogoro Bw. Jacob Kayange amebainisha kuwa jukumu kubwa la waandikishaji hao ni kuandikisha wananchi wenye sifa za kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa huku akisema kuwa vituo vya uandikishaji na kupiga kura vitakuwepo katika kila kitongoji.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Msimamizi wa Uchaguzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Bi. Mary Kayowa amemuahidi Katibu Tawala huyo kuwa Mvomero imejipanga kuhakikisha kuwa maelekezo, miongozo na taratibu inasimamiwa ipasavyo ili zoezi hilo lifanyike kwa ufanisi. Aidha, ameongeza kuwa mafunzo hayo yalianza Oktoba 07 kwa washiriki kutoka Tarafa za Mvomero na Turiani huku akibainisha kuwa kwa Tarafa za Mgeta na Mlali zinajumla ya washiriki 371.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RUWASA MVOMERO YAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI YA MAJI KWA UFANISI

    April 13, 2025
  • MWENGE WA UHURU KUMULIKA MIRADI YA MAENDELEO 7 YENYE THAMANI YA TSH. 1.06 WILAYANI MVOMRO

    April 13, 2025
  • DC MVOMERO AAGIZA SHULE SHIKIZI MINGO ISAJILIWE, IPOKEE WANAFUNZI JANUARI 2025

    March 27, 2025
  • KUU MVOMERO YAKISHUKURU KIWANDA CHA SUKARI MTIBWA KWA KUSAIDIA WANANCHI KURUDISHA MTO KWENYE MKONDO WAKE

    March 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.