• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

RAIS SAMIA ASIKIA KILIO CHA WAFUGAJI, ATOA SH. BILIONI 216 KUBORESHA SEKTA YA MIFUGO KWA MIAKA 5

Posted on: July 10th, 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameonesha dhamira thabiti ya kuboresha maisha ya wafugaji nchini kwa kutoa Shilingi Bilioni 216 kwa ajili ya kuimarisha sekta ya mifugo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo hadi mwaka 2029.


Hayo yamebainishwa Julai 10, 2025 na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji wakati akizungumza na wananchi kwenye hafla ya uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya chanjo na utambuzi wa mifugo katika Mkoa wa Morogoro, iliyofanyika katika Kijiji cha Kambala Wilayani Mvomero.


Waziri huyo wa Mifugo na Uvuvi, amesema kuwa fedha hizo zitatumika kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa kampeni ya chanjo na utambuzi wa mifugo, ununuzi wa vishikwambi, pikipiki kwa ajili ya maafisa mifugo ambapo kwa mwaka huu jumla ya shilingi bilioni 69.2 zimetolewa kwa ajili ya kufanikisha zoezi hilo.


“...mama karidhia sasa tutekeleze mpango wa uboreshaji wa Sekta ya mifugo kwa miaka mitano mfululizo na tunaanza na mwaka huu 2025...2029 tutahitimisha mpango wa maboresho kimapinduzi sekta ya mifugo...” amesema Waziri Kijaji.


Aidha, amebainisha kuwa kampeni hiyo ya chanjo Pamoja na utambuzi linafanyika nchi nzima ambapo jumla ya ng’ombe milioni 19, mbuzi na kondoo milioni 17 na kuku milioni 40 watatambuliwa na kuchanjwa huku akiwataka wafugaji kujitokeza kwa wingi ili mifugo yao iweze kupata chanjo.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Maulid Dotto akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema kuwa Mkoa huo umepokea chanjo ya CBPP 707000 kwa ajili ya ng’ombe 815,051, chanjo ya PPR 847,500 kwa ajili ya mbuzi na kondoo 737,673 na chanjo ya kuku 999000 kwa ajili ya kuku 1,654,617. Ameongeza kuwa jumla ya heleni 188000 kwa ajili ya ng’ombe na heleni 177500 kwa ajili ya mbuzi na kondoo.


Kwa upande wake Chifu Kashu Moreto ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutimiza suala la chanjo na utambuzi wa mifugo hukua akisema kwa wamelipokea kwa mikono miwili.


MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.