• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

RAIS SAMIA AENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA MVOMERO, ATOA MILIONI 50 KUMALIZIA ZAHANATI YA KIJIJI CHA MAFURU

Posted on: January 17th, 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuonyesha dhamira ya serikali yake katika kuboresha huduma za afya nchini kwa kutoa shilingi milioni 50 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Mafuru, Wilayani Mvomero.

Hayo yamebainishwa Januari 17 mwaka huu na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mwl. Linno Mwageni wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mafuru alipotembelea kukagua jengo la zahanati ambalo limefikia hatua ya lenta ikiwa ni nguvu za wananchi.

Mwl. Linno amewapongeza wananchi wa kijiji hicho kwa kuwa na wazo la kujenga zahanati huku akibainisha kuwa fedha zilizotolewa na Serikali ni kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za wananchi hao zitatumika kwa ujenzi wa miundombinu iliyosalia na kuhakikisha zahanati hiyo inaanza kutoa huduma haraka iwezekanavyo.

"...niwapongeze kwanza kwa kuwa na wazo la kuwa na zahanati na mkaanza boma...Serikali tukufu inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeleta mzigo hapa, milioni 50 ili kukamilisha zahanati ianze..." amesema Mwl. Linno.

Aidha, Mkurugenzi huyo amewataka wananchi kuhakikisha kuwa fedha hizo zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na kwamba Zahanati ijengwe kwenye kiwango kinachohitajika ili kuhakikisha kuwa zahanati inaanza kutoa huduma kuanzia mwezi Julai mwaka huu.

Sambamba na hilo, Mwl. Linno ameuagiza uongozi wa kijiji hicho kuhakikisha inaunda kamati ya ujenzi itakayokuwa imara ili mradi ukamilike kwa wakati na sio kwenda kutumia fedha hizo vibaya.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo amewataka wananchi kuzingatia kanuni za usafi wa mazingira ikiwemo matumizi sahihi ya vyoo huku akiwataka kutumia maji yaliyochemshwa ili kujikinga na magonjwa ya kuhara na kutapika.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dkt. Philipina Philipo amesema Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo imetoa shilingi milioni 50 ambazo tayari zimeingizwa kwenye akaunti ya kijiji kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa zahanati hiyo ambayo itasaidia kuwaondolea wananchi adha ya kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya maeneo mengine.

Pamoja hayo, Dkt. Philipina amewakumbusha wananchi kuendelea kuzingatia kanuni za usafi wa mazingira kama kunawa mikono kwa maji safi, kuchemsha maji kabla ya kuyatumia hususan kipindi hiki ambacho mvua zinanyesha ili kujikinga na magonjwa ya kuhara.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Mafuru ameishukuru Serikali kwa kuleta fedha kwa ajili ya umaliziaji wa zahanati hiyo, pia amesema Kijijini hapo mifugo bado inasumbua kwenye mashamba ya wakulima na kupelekea wananchi kushindwa kujitoa kwenye kazi ya ujenzi kwa sababu wanatumia muda mwingi kulinda mashamba yao.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.